![]()
![]()
10 Comments
WAHUSIKA WADOGO
Salome na Mina: Wahusika wadogo ambao wanatajwa tu. Hawashiriki moja kwa moja katika masuala ya tamthilia hii. Salome ni mwanawe Yona na Mina ni bintiye Bunju na Neema.
Umuhimu wao
Wanakamilisha idadi ya watoto wa Yona na Bunju mtawalia. Idadi hii ni dhihirisho la usasa ambapo wazazi hawapati watoto wengi kutokana na hali ibuka za kiuchumi na za kijamii. Pia, wanaendeleza malezi ya kisasa ambapo watoto hawaonani na wazazi wao kwa kuwa wanahudhuria masomo ya bweni au nje ya nchi.
Ushauri muhimu kwa mtahiniwa
LemiNi mvulana wa miaka kumi, mwanawe Bunju. Sifa zake:
Umuhimu wakeLemi anawakilisha watoto wa baadhi ya wazazi ambao hawapati wakati mwingi wa kuingiliana na wazazi wao ambao mara mwingi wako kazini. Anawakilisha watoto ambao hulelewa na yaya.
BelaNi mfanyakazi wa nyumbani wa Neema. Sifa zake:
Umuhimu wakeAnawakilisha wafanyakazi wa kiwango cha chini wanaowajibika, kuheshimu na kuthamini kazi zao.
BeniMwanakijiji ambaye ni jirani na rafikiye Yona. Sifa zake:
Umuhimu wakeNi hasidi katika jamii. Watu wa aina hii huwachochea wenzao na mwisho kuwatenganisha na wake na familia zao. Yona anapuuza uchochezi wa Beni na kuonyesha kuwa sasa ameanza kupatwa na mwamko mpya.
LukaMwanakijiji ambaye ni jirani na rafikiye Yona. Sifa zake:
Umuhimu wakeAnadhihirisha kwamba hata vijijini mabadiliko ya kimawazo kuhusu mtoto wa kike yameanza kukita mizizi. Anamchora Neema kama "simba wa kike" (uk. 67).
KiwaKijana wa kiume, mtoto wa Dina. Kama majirani wengine anashangazwa na bidii za watoto wa Sara na Yona. Sifa zake:
Umuhimu wake
DinaNi mama wa umri wa makamu na jirani wa Sara na Yona. Sifa zake:
Umuhimu wake
BunjuBunju ni mumewe Neema. Sifa zake:
Umuhimu wake
AsnaBintiye Yona wa pili. Ni mdogo wake Neema. Asna ni mhusika msaidizi. Anamsaidia msomaji kuelewa baadhi ya masuala yanayojadiliwa katika tamthilia. Sifa zake:
Umuhimu wake
NeemaNeema ambaye ni binti wa Yona na Sara ni mhusika mjenzi. Neema ni mke wa Bunju. Wasifu wa Neema unadhihirika kutokana na kauli zake na za watu wengine pamoja na matendo yake. Neema anadhihirisha sifa kadhaa: SIFA ZAKE:
Umuhimu wake
SaraSara ni mke wa Yona. Yeye pia ni mhusika mkuu kwa sababu anahusika na karibu masuala yote ya tamthilia hii. Ndoa yake ilikuwa na changamoto nyingi zikiwemo mahitaji ya kiuchumi, fujo za mumewe ambaye alikuwa akishiriki ulevi na ugonjwa wa moyo uliomkaba. Sifa zake:
Umuhimu wake
WAHUSIKAYonaNi mume wa Sara na pia ni mmoja wa wahusika wakuu. Anatambulika kama mhusika mkuu kwa sababu anahusika na takriban masuala yote yanayojadiliwa katika tamthilia hii. Ni kama kwamba kila kitu katika tamthilia hii kinamhusu. Sifa zake:
Umuhimu wake
Taharuki
Mifano
SadfaSadfa katika fasihi ni hali ambapo matukio mawili hutokea kwa wakati mmoja bila kupangwa na kwa namna ya kushangaza au inayoashiria bahati. Mbinu ya sadfa imetumiwa mara kadhaa katika tamthilia ya Bembeaya Maisha.
Mbinu rejeshi
Usemaji-kando
MBINU ZA KIMUUNDOMbinu za kimuundo hutumiwa na mwandishi kuendeleza msuko wa kazi ya fasihi. Mwandishi wa tamthilia ya Bembea ya Maisha ametumia mbinu kadhaa za kimuundo kujenga msuko wa tamthilia yenyewe. MifanoUzungumzi nafsiaNi aina ya monolojia itolewayo na mhusika mmoja akiwa jukwaani pekee yake. Mbinu hii hutumiwa kuwasilisha maoni, hisia na fikra za mhusika kuhusu jambo fulani.
TanakuziNi tamathali ya usemi inayolinganua mawazo kwa kutumia mkinzano wa maneno, virai au sentensi kwenye miundo yenye usambamba.
TabainiNi mbinu ya fasihi ambapo jambo husisitizwa kwa kutumia kikanushi 'si'. Mbinu hii imetumiwa na mwandishi wa Bembea ya Maisha mara kadhaa. Mifano:
Ishara na taashiraIshara katika fasihi hutumiwa kurejelea kitendo, hali au kitu kinachodokeza au kuonyesha dalili ya kitu kingine. Nayo taashira ni alama mahususi ambazo huhusishwa na hali fulani katika jamii.
MBINU ZA KISHAIRIMbinu za kishairi ni sehemu muhimu ya matumizi ya lugha katika tungo za kitamthilia. Miongoni mwa mbinu hizo muhimu ni takriri. TakririTakriri ni urudiaji wa sauti, silabi, neno au sentensi za namna moja zinazofuatana kwa karibu. Takriri hupamba lugha katika fasihi na pia kuvuta nadhari ya msomaji au msikilizaji. Mwandishi wa tamthilia ya Bembeaya Maisha ametumia mbinu ya takriri katika kazi yake. Mifano:
Tashihisi ni mbinu ya mwandishi kuvipa viumbe visivyo na uhai sifa za uhai au za kibinadamu. Pia huitwa uhuishi
Ni mbinu ya lugha inayotumia ulinganisho wa moja kwa moja wa kitu na kingine. Kitu kimoja husemwa kuwa kingine. Mifano ya sitiari katika tamthilia ya Bembea ya Maisha.
Methali ni aina ya semi ambayo huwa na muundo maalumu. Hueleza ukweli fulani wenye maana pana na unaoweza kufasiriwa kwa njia mbalimbali. Methali hukusudia kuonya, kuelekeza, kuadhibu, kusuta, kulaumu, kushauri na kadhalika. Methali huwa imebeba maana pana kuliko maneno yenyewe. Tamthilia ya Bembea ya Maisha imetumia mbinu ya methali kwa wingi. Mifano:
Methali katika tamthilia ya Bembea ya Maisha zimetumika kutekeleza yafuatayo:
|
Bembea ya Maisha ni hadithi kuhusu Yona na mkewe Sara pamoja na Bunju na mkewe Neema. Wahusika hawa wanajikuta katika vuta n’kuvute inayochochewa na mitazamo ya kitamaduni, uhalisia wa mambo pamoja na matamanio ya wahusika binafsi. Baina yao kuna mitikiso inayotishia familia, ndoa na mahusiano ya kijamii. Kuna shutma, shaka, tuhuma na mivutano. Lakini pia kuna hongera, imani, ushirikiano, upendo, kutanabahi na mshikamano. Katika huu mseto wa mambo ipo sauti imara ya Sara inayosikika ikihimiza na kuzindua. Sauti inayoiona kila hali mfano wa bembea.
AuthorAtika School Team Archives
September 2023
Categories
All
|