ATIKA SCHOOL
  • Start
    • Help & Support >
      • About Us
    • Academic Environment
    • KNOWLEDGE CENTRE
    • How its Done
    • NICHE PAGES >
      • The Constitution of Kenya, 2010
      • Atika School Short Stories for 7-12 Years Learners
      • KNEC Portal
      • ZERAKI HELP AND SUPPORT
      • KNEC KCSE PROJECT INSTRUCTIONS
      • JOBS IN KENYA AND ABROAD FOR KENYANS AND BEYOND
  • MEMBERS PORTAL
  • BLOGS
    • QUESTIONS & ANSWERS >
      • SECONDARY >
        • LANGUAGES >
          • Secondary English Questions and Answers
        • TECHNICALS >
          • COMPUTER STUDIES >
            • KCSE Computer Studies Questions and Answers: Comprehensive Analysis and Resources
            • kcse computer studies paper 2 AND 3 Questions & Answers
          • BUSINESS STUDIES QUESTIONS & ANSWERS
          • KCSE AGRICULTURE TOPICAL QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCSE HOME SCIENCE DIRECT QUESTIONS AND ANSWERS
        • SCIENCES >
          • KCSE Mathematics Topical Questions
          • KCSE Biology Topical Questions and Answers
          • CHEMISTRY TOPICAL QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCSE Physics Topical Questions
          • KCSE physics Practical Sample Quiz
        • HUMANITIES >
          • ATIKA SCHOOL - KCSE CRE Questions and Answers
          • ISLAMIC RELIGIOUS EDUCATION (IRE) QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCSE History Topical Questions and Answers
          • GEOGRAPHY TOPICAL QUESTIONS AND ANSWERS
      • PRIMARY >
        • Standard 4-8 Mathematics Topical Questions from Mocks and KCPE
        • Std 6 Mathematics Notes
    • TUTORIALS >
      • SECONDARY >
        • SCIENCES >
          • FOCUS MATHEMATICS TUTORIALS AND EXAMS FREE
          • KCSE BIOLOGY NOTES
          • FREE KCSE CHEMISTRY NOTES
          • KCSE PHYSICS NOTES, AUDIOVISUALS AND MORE
        • LANGUAGES >
          • ENGLISH >
            • FATHER OF NATIONS STUDY GUIDE
            • A GUIDE TO SILENT SONG AND OTHER STORIES
            • English KCSE Set Books
            • ENGLISH POETRY QUESTIONS WITH ANSWERS FOR K.C.S.E CANDIDATES
            • KCSE English Grammar: A Comprehensive Guide for Students
          • KISWAHILI >
            • Bembea ya Maisha
            • CHOZI LA HERI - MWONGOZO
            • KIGOGO - MWONGOZO
            • MASWALI NA MAJIBU YA TUMBO LISILOSHIBA
            • USHAIRI MASWALI NA MAJIBU
            • KCSE Kiswahili Fasihi
        • TECHNICALS >
          • COMPUTER STUDIES NOTES LATEST
          • HOME SCIENCE NOTES
          • KCSE BUSINESS STUDIES NOTES
          • KCSE AGRICULTURE NOTES, SYLLABUS, QUESTIONS, ANSWERS, SCHEMES OF WORK AND OTHERS
        • HUMANITIES >
          • KCSE History Notes Form 1 to 4
          • FREE KCSE CRE NOTES
          • KCSE GEOGRAPHY NOTES
          • IRE NOTES, AUDIOVISUAL, QUESTIONS AND ANSWERS
      • PRIMARY >
        • STANDARD 4: SOCIAL STUDIES
        • NOTES >
          • KISWAHILI
          • SOCIAL STUDIES
        • EXAMINATIONS
        • DecaTurbo Online Series Examinations
        • KCPE Mathematics Notes
        • KCPE and Primary Level Compositions
      • Other Supportive Documents >
        • SYLLABUS >
          • Primary 8-4-4 based Syllabus, Objectives and Lessons
          • Primary Mathematics Syllabus
        • MASOMO VIDEOS
    • EXAMINATIONS >
      • MOCKS AND JOINT EXAMS >
        • FORM 1 QUESTION PAPERS, ANSWERS AND MARKING SCHEMES COLLECTIONS
        • FORM 2 QUESTION PAPERS, ANSWERS AND MARKING SCHEMES COLLECTIONS
        • FORM 3 EXAMINATIONS, QUESTION PAPERS AND ANSWERS
        • FORM 4 MOCKS PAST EXAMS BY REGION
        • TOP SECONDARY EXAMS ALL SUBJECTS
      • KPSEA NATIONAL EXAMS
      • KCPE >
        • KCPE PAST PAPERS AND ANSWERS >
          • KCPE 2020 RESULTS, REPORTS, QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCPE PAST PAPERS 2019 REPORTS, RESULTS, QUESTIONS AND ANSWERS
        • KCPE PAST PAPERS PER SUBJECT
      • KCSE >
        • KCSE PAST PAPERS BY SUBJECT
        • KNEC KCSE PAST PAPERS, MARKING SCHEMES, QUESTIONS & ANSWERS
        • Free KCSE Past Papers Mathematics
        • Free KCSE Biology Questions and Answers
  • OUR PRODUCTS
    • All Categories >
      • MORE PRODUCTS >
        • SECONDARY CRE NOTES
        • COURSE BOOKS
        • KCSE KISWAHILI SETBOOKS
        • Backed Up Files and Archives
        • FREE DOCUMENTS
        • PRIMARY 8-4-4 BASED RESOURCES
        • STANDARD 8 RESOURCES
        • HIGH SCHOOL RESOURCES >
          • Biology Paper 3 Exams
          • Secondary Examinations
        • PRIMARY CBC BASED RESOURCES
        • COLLEGE & VARSITY RESOURCES
      • PRIMARY RESOURCES CBC
      • PRIMARY RESOURCES 8-4-4
      • SECONDARY RESOURCES
      • NOTES & TUTORIALS
      • COLLEGE RESOURCES
      • NOVELS and OTHER BOOKS
    • CURRICULUM >
      • NEW CURRICULUM DESIGNS >
        • PRIMARY >
          • PRE PRIMARY ONE CURRICULUM WITH SYLLABUS
          • PRE PRIMARY TWO CURRICULUM WITH SYLLABUS
        • SECONDARY >
          • KNEC KCSE SYLLABUS AND COURSE OUTLINES
        • COLLEGE >
          • Regulations for the TIVET Craft and Diploma Business Examinations
    • HIGH INSTITUTIONS >
      • EXAMINATIONS >
        • College and Varsity Past Papers online
      • TUTORIALS >
        • COLLEGE AND UNIVERSITY NOTES AND TUTORIALS

MWONGOZO WA TAMTHILIA YA KIGOGO NA PAULINE K.K Tamthilia ​(2017-2021)

utawala mbaya ni tatizo  sugu  linalozikumba nchi nyingi za kiafrika; Jadili kwa kurejelea  matukio ishirini katika tamthilia ya kigogo.(al 20)

1/2/2023

0 Comments

 

​utawala mbaya ni tatizo  sugu  linalozikumba nchi nyingi za kiafrika; Jadili kwa kurejelea  matukio ishirini katika tamthilia ya kigogo.(al 20)

  • uongozi ume salia katika familia moja ya kina majoka  tangu uhuru ulipopatikana.
  • badala ya kupiga vita pombe haramu ,serikali inatoa kibali cha kuuza pombe kinyume na sheria
  • badala ya kulinda usalama polisi wanatumiwa kutawanya  na kuwapiga watu wanaoandamana
  • Viongozi wa upinzani ambao wanapinga utawala wa kiimla  wa majoka wanauwawa km jabali
  • majoka ana unafiki kwani  anasema wasiruhusu  watu wachache waliojazwa kasumba za kikoloni kuwarejesha katika utumwa
  • majoka anapanga kuongeza mishahara walimu na wauguzi  kisha wapandishe kodi 
  • serikali inakopa pesa  nyingi  kugharamia miradi duni kama kuchonga vinyago
  • serikali inashiriki katika biashara ya kukata na kuuza miti  badala ya kutunza mazingira
  • majoka  anatumia ushirikina  katika uongozi wake ,nembo ya chama chake swila /nyoka
  • majoka and majoka company  inatengeneza dawa za kulevya  na kuharibu vijana kama ngao junior
  • majoka anaagiza watu kusherehekea uhuru wa jimbolao la mwezi mmoja

10x2
Mwalimu akadirie

Read More
0 Comments

‘Shika hamsini zako wewe…Hatutaki  kufanya nira na mtu…’

1/2/2023

0 Comments

 

​a) Eleza muktadha wa dondoo hili ( al4)

Mnenaji ni Boza, mnenewa ni Sudi,mahali ni karakanailiyoko sokoni chapakazi.Kenga   alikuwa  amewaletea keki ya uhuru  naye Sudi  akakataa kuila  kwani  anaiona  kama masazo kwa sababu  ile nzuri imeliwa kwingine

​b) eleza tamathali ya usemi  uliotumika (al2)

​msemo:
shika hamsini zako 
hatutaki kufunga nira

​c) uongozi wa majoka  umesheheni sumu ya nyoka.Thibitisha kauli hii kwa kudokeza hoja saba (al14)

  • Majoka anawaua wapinzani wake wa kisiasaili kuzuia mapingamizi
  • majoka alifunga soko la chapakazi  na kuwafanya watu wateseke,ashua na sudi
  • sumu ya nyoka inayotengenezwa  na kampuni ya majoka inapenya shuleni, wanafunzi wanaitumia na hivyo kuwafanya makabeji.
  • majoka anamfungia ashua gerezani  ili kumlazimisha sudi amchongee kinyagocha ngao
  • uongozi wa majoka unasambazavijikaratasi kuwachochea watu kuhama sagamoyo.
  • majoka anawapa polisi kibali cha kuwashambulia waandamanaji ,jambo linalowapelekea vijana watano kuuliwa
  • majoka anamfuta kingi kazi baada ya kukaidi amri yake ya kuwa fyatua watu risasi 
7x2
Mwalimu akadirie jibu 


Read More
0 Comments

“ Do!Do!Si mameni !Si mameni ! leo kutanyesha mawe!“

25/12/2022

0 Comments

 

“ Do!Do!Si mameni !Si mameni ! leo kutanyesha mawe!“

maswali

i . Eleza muktadha wa dondoo hili    ( Alama 4)
ii. Fafanua mbinu za lugha zilizotumika katika dondoo hili    ( alama 4
iii . Huku ukitoa mifano jadili  hoja sita zinazodhihirisha jinsi mwanamke alivyasawiriwa katikaTamthilia ya Kigogo   ( alama 12)

majibu

​Ni maneno yaNgurumo
Anawaambia walevi wenzake
Wako Mangweni kwa Mamapima/Asiya
Anayasema maneno haya anapowaonaTunu na Sudi kwa mamapima ,jambo ambalo halikuwa la kawaida.  (al 4)             

i. Nidaa-  Do! Do ! Do!
  • Takriri - Simameni!   Simameni! Simameni!
  • Jazanda -    Kutanyesha mawe(al 4)

ii.
  • Mteteziwahaki-Tununa Asha wanatetea haki za Wanasagamoyo
  • Jasiri- Tunu anamkabili Majoka bila uoga
  • Msomi- Tunu anasomea uanasheria
  • Ashua amesomea ualimu
  • Chombo cha burundani/ Kustareheka- Majoka anapomwona Ashua akiingia ofisini mwake anaona kuwa amerudi kwake kuonja asali.
  • Mbeya- Ashua anamkejeli Husda kuwa ana  sifa ya umbeya iwe hadharani ama faraghani.
  • Mzalendo- Tunu analipenda jimbo anapopigania mabadiliko yatakayowafaa Wanasagamoyo .
  • Mwasherati/ Asherati- Asiya ana uhusiano wakimapenzi na Ngurumo ilhali yeye ni mke wa Boza.
  • Pia anahusishwa na Keki za Uroda.
  • Mpenda anasa na starehe-  Husda hupenda kwenda kwenye hoteli ya kifahari kujivinjari.
  • Mpyoro/mwenye matusi- Husda anamtusi Ashua kwa kumwita hawara, kidudu mtu na mbeya.
Mwenye msimamo dabiti   
(zozote 12X1=12) 

Read More
0 Comments

​“ Sitaki kazi za uchafu hapa …”

25/12/2022

0 Comments

 

​“ Sitaki kazi za uchafu hapa …”

(a) Eleza muktadha wa dondoo (alama 4)

(a)
​Msemaji- Majoka
Msemewa- Ashua
Mahali- Ofisini kwa Majoka
Kiini- Baada ya Ashua kuoimba msaada kwa sababu wanawe walilala njaa
4x1

(b) Kwa kurejelea hoja kumi, onyesha jinsi kinaya inajitokeza katika tamthiliya (alama 10)

(b)
(i) Soko ni chafu-maji ya povu kwenye mtaro
(ii) Anamtaka Ashua mapenzi ilhali ana mke. Huu ni uchafu wa kimaadili.
(iii) Wanafunzi wa Majoka and Majoka Academy hawafuzu- kuwa makabeji kutokana na sumu ya nyoka
(iv) Ngurumo kuzikwa juu ya maiti wengine
(v) Kenga kumsaliti Majoka
(vi)Majoka kuwakuta watu achache kwenye lango la soko
(vii) Akina Kombe na Boza kupewa makombo ya keki ilhali wao ndio wanazalisha (rasilimali inatumiwa kwingine)
(viii) Kulipa kodi na kitu juu yake
(ix) Majoka anaamrisha mauaji ya Jabali na raia wengine ( mikono yake ni michafu-ina damu)
(x)Mamapima kupewa kibali cha kuuza pombe haramu
10x1
Mwalimu akadirie kazi ya mwanafunzi

(c ) Fafanua sifa sita za msemaji (alama 6)

​(c)
​(i) Katili
(ii) Mkware
(iii) Mwenye tamaa-mali
(iv) Mwenye dharau- zebe wako
(v) Mpyoro
(vi) Mbinasfi
(vii) Mfisadi 6x1
Lazima mwanafunzi aeleze ndiposa apewe alama kamili.
Mwalimu akadirie kazi ya mwanafunzi

Read More
0 Comments

​“ASANTE YA PUNDA KWELI NI MATEKE, SIKUJUA UNGEKUJA KUNIHANGAISHA HIVI”.

24/12/2022

0 Comments

 

​“Asante ya punda kweli ni mateke, sikujua ungekuja kunihangaisha hivi”. 

​ a) Eleza muktadha wa dondoo hili.  (Al 4)

Eleza muktadha dondoo hili
  1. Haya ni maneno ya majoka.
  2. Anamwambia Tunu
  3. Wamo ofisini mwa majoka 
  4. Majoka anajuta kwa kugharamia masomo ya Tunua ambaye amekuja sasa kumhangaisha kwa kupinga utawala wake dhalimu

​b) Fafanua tamathali ya usemi katika dondoo hili    (Al 2)

​c) Kauli hii ina maana gani kwa mujibu wa muktadha huu  (Al 2)

Kauli hii ina maana gani kwa mujibu wa muktadha huu? 
Majoka anajuta kwa kugharamia masomo ya Tunu ambaye sasa amekuja kumhangaisha kwa kupinga utawala wake.

​d) Onyesha jinsi anayeambiwa maneno haya anavyoangaisha mzungumzaji.  (Al 4)

Onyesha jinsi anayeambiwa maneno haya anavyomhangaisha mzungumzaji
  1. Baada ya Majoka kufunga soko la chapakazi , Tunu anaongoza maandamano ya kupinga
  2. Baada ya Majoka kumuua jabali, kiongozi wa upinzani kwa ajali, Tunu anaaanza kupanga mikakati ya kuwaleta wachunguzi wa nje ili kuitathmini ajali hiyo upya, jambo linalomtia Majoka wasiwasi. 
  3. Tunu anawaongoza raia kususia sherehe za kuadhimisha uhuru wa sagamoyo ambazo zingeongozwa na Majoka – Majoka anaishia kuaibika anapofika katika uwanja wa ikulu akiwa na wageni wake na kupata kwamba ni raia kumi tu waliokuwa wamekuja kuhudhuria sherehe hiyo. 
  4. Baada ya kuwaongoza raia kususia sherehe za uhuru ambazo zingeongozwa na Majoka, Tunu  anawahutubia raia na kuwachochea dhidi ya uongozi wa Majoka. Anawahimiza kumchagua kiongozi anayefahamu fika kadhia zao; njaa na kilio chao. 
  5. Baada ya Majoka kubomoa vioski vilivyoko kwenye soko la chapakazi, Tunu anamwendea hadi ofisini mwake na kumhakikishia kwamba hatajenga hoteli yake mahali hapo.
  6. Baada ya  Majoka kufunga soko na kufuja pesa za kusafisha soko hilo, Tunu anawahutubia waandishi wa habari na kumkashifu kwa matendo hayo. 
  7. Asilimia sitini ya raia inataka kumpigia kura Tunu kutokana na juhudi zake za kuwatetea, jambo linalomtia Majoka tumbojoto.

​e) Jadili jinsi hali ya “Asante ya punda ni  mateke” inawaafiki wanasagamoyo.(Al 8)

​Jadili jinsi ambavyo hali ya “asante ya punda ni mateke” inawaafiki wasagamoyo
  1. Majoka anagharimia msomo ya  Tunu ilhali Tunu anakuja kumhangaisha kwa kuupinga uongozi wake kwa sababu ya kuwadhulumu raia, kwa mfano, kufunga soko.
  2. Mumewe hashima anamfanyia Majoka kazi katika kampuni yake lakini anapokufa Majoka anataka kumnyima mkewe; Bi. Hashima fidia kwamba hawakuwa na bima. 
  3. Kombe ni mfuasi sugu wa mrengo wa Majoka lakini serikali ya Majoka inasambaza vikaratasi ikiwataka watu kutoka katika kabila lake kuhama sagamoyo kwa madai kwamba si kwao. 
  4. Chochote anachoambua sudi katika kazi yake huwa anamleta mkewe Ashua lakini Ashua haridhiki kwa sababu ya kutaka kuishi  yasiyo yake. Anateta kuwa sudi hampi hata masurufu. 
  5. Majoka anampa kenga kazi kw kumchagua kuwa mshauri wake mkuu lakini raia wanapoandamana kupinga kufungwa kwa soko, anaungana nao kumg’oa uongozini. 
  6. Chopi anamtii Majoka kwa kufanya kila analomuagiza lakini anataka kumuua kwa kosa moja pekee – kutohakikisha kuwa Tunu amepigwa na kuuliwa jinsi alivyokuwa amemuagiza. 
  7. Kuna vijana watano wanaomfanyia Majoka kazi katika Majoka and Majoka company lakini wanauliwa wanapoandamana kupinga kuongezwa kwa bei ya chakula kwenye kioski cha kampuni. 
  8. Tunu anajitolea kuwatetea raia dhidi ya dhuluma za Majoka lakini raia wenzake kama Ngurumo wanakubali kutumiwa na Majoka kumvamia na kumuumiza – anaumizwa mfupa wa muundi. 
  9. Walimu na wauguzi wanalitumikia jimbo la sagamoyo lakini serikali inawalipa mshahara duni, hali inayowasabibishia kugoma na kuandamana. 
  10. Raia wanaimba nyimbo za kusifu utawala na babuye Majoka (Ngao) lakini Majoka anawadhulumu kwa kulifunga soko wanaolitegemea badala ya kuboresha maisha yao kwa maaana wanausifu uongozi wa familia yao. 
  11. Sudi anadhihirisha mapenzi kwa mkewe, Ashua kwa kumwita baby, honey nan a sweetie lakini Ashua anataka talaka, hali inayotishia kuvunja ndoa yao. 
  12. Boza na kombe wanakubali kumchongea Majoka kinvago cha babuye Ngao lakini Majoka analifunga sokoambapo wanachongea na kuuzia vinyago vyao, hivyo kuathiri biashara zao. 
  13. Wafanyibiashara kama Ashua wanatii agizo la serikali la kutoa kodi lakini Majoka hawasafishii soko, hivyo kuishia kufanya biashara zao katika mazingira machafu licha ya kulipa kodi. 
  14. Ngurumo ni mfuasi sugu wa Majoka lakini Ngurumo anapokufa Majoka hahudhurii maziko yake. Anatoa Maagizo kwamba azikwe juu ya wafu wengine kwa sababu maziara yalikuwa yamejaa. 
  15. Sudi anawafungulia Boza na Kombe kiredio chake kwenye rununu yake wasikilize hukuwakichonga vinyago lakini sudi anapokizima, Boza anaanza kumtusi kwa kumwambia kwamba kirununu chake cha pesa nane kimsimtie kiburi.
  16. Wananchi wanawapeleka wanao katika shue ya Majoka and Majoka Academy , hivyo kumtajirisha Majoka kutokana na karo wanayolipa lakini wanafunzi hao wanaruhusiwa kutumia dawa za kulevya badala ya kusoma, hivyo kuishia kuanguka mtihani. 
  17. Raia wanamchagua Majoka kuwa kiongozi wao lakini anawadhulumu kwa kuwaua baadhi yao na kulifungua soko wanalolitegemea. 
  18. Boza anamruhusu Ngurumo kupika pombe haramu na mkewe, Mamapima lakini Ngurumo anamsaliti Boza kwa kuzini na mamapima.

Read More
0 Comments

​TATHMINI MAUDHUI YA NDOA KWA MUJIBU WA TAMTHILIA YA KIGOGO.    (AL 20)

24/12/2022

0 Comments

 

​Tathmini maudhui ya ndoa kwa mujibu wa tamthilia ya kigogo.    (Al 20) 

​Tathmini maudhui ya ndoa kwa mujibu wa tamthilia ya “Kigogo”
  1. Wanandoa wanasaidiana katika kuzikimu familia zao kwa kufanya kazi wote – kwa mfano, sudi na mkewe Ashua wafanya biashara katika soko la Chapakazi ili kujikimu kimaisha. 
  2. Baadhi ya wanandoa wanapendana – Kwa mfano, Ashua anapompelekea mumewe sudi chai na mahamri sokoni, Sudi anasimama na kumkumbatia. Aidha sudi anamwita mkewe Ashua honey na sweetie, akiwa kwenye chumba cha wafungwa. 
  3. Baadhi ya wanandoa si waaminifu – Kwa mfano, Asiya/mamapima anazini na Ngurumo ilhali ana mumewe, Boza. Isitoshe, hata Ngurumo ana mkewe. Hata Majoka anamwendea kinyume mkewe Husda kwa kutaka kuzini na Ashua.
  4. Baadhi ya ndoa hazina mapenzi ya kweli – kwa mfano, majoka anapozirai anazungumza na mkewe Husda na kumwambia kuwa hampendi kamwe na kumwambia kwamba ampendaye ni Ashua; mkewe sudi. Aidha Majoka anadai kwamba hata mkewe Husda hampendi/anachopenda ni mali zake. 
  5. Ndoa inakabiliwa na tatizo la unafiki – Majoka anabainisha kwa husda anajifanya kuwa anampenda (Majoka) bali anachokipenda ni mali zake. 
  6. Ndoa imekumbwa na  tatizo la ujane – Bi. Hashima anabaki mjane baada ya kufiwa mumewe. 
  7. Baadhi ya wanandoa wana tamaa ya mapenzi nje ya ndoa – Majoka anatamani Ashua, mkewe sudi, ilhali ana mkewe. Isitoshe, naye Husda anatamani Chopi kwa kumtazama kwa macho ya uchu ilhali ana mumewe, Majoka. 
  8. Uchochezi ni chanzo ya kuvunjika kwa ndoa -. Ashua anamwomba mumewe, sudi talaka baada ya Majoka kumchochea dhidi yake, hali inayotishia kuvunjika kwa ndoa yao. 
  9. Baadhi ya wanamume wanawadhulumu wake wao – kwa mfano, Husda anapozua rabsha ofisini baada ya kumkuta majoka na Ashua, Majoka anamwambia kuwa angeleta fujo angemchafua. 
  10. Mwanaume ambaye ameoa na anatembea na mwanamke ambaye hajaolewa ni tishio la kuvunjika kwa ndoa, kwa mfano, Ashua anamtaka mumewe sudi kumpa talaka kwa sababu ya kutembea na Tunu mara kwa mara ilhali Tunu hajaolewa; hivyo kumshuku kuwa mpenziwe. 
  11. Baadhi ya wanawake wanawataabisha wanaume kwa kutoridhika na wanachopewa na wanaume wao. Kwa mfano, Sudi anampa mkewe Ashua kila anachokiambua lakini Ashua haridhiki. Anataka Zaidi ya uwezo wa sudi hali ambayo imeleta mgogoro baina yao. 
  12. Wanawake ni wasaliti katika ndoa – Ashua anamsaliti mumewe sudi kwa kumwambia kwamba amechoka kupendwa kimaskini ilhali anajua kwamba kipato cha sudi si kikubwa kwa sababu anafanya kazi duni ya kuchonga vinyago sokoni Chapakazi. 
  13. Wanaume wanatoa ahadi za uwongo kwa wanawake wakati wa kuchumbiana – Kwa mfano, Sudi alimuahidi Ashua mengi kabla ya kumwoa lakini hakuyatimiza hali inayomchochea Ashua kutaka kuivunja ndoa yake. 
  14. Baadhi ya wanandoa ni waaminifu – Kwa mfano, Ashua anakataa kufanya mapenzi na Majoka kwa kumwambia kuwa yeye ni mke wa mtu (sudi)
  15. Jukumu la mwanamke limedhiririka katika ndoa – kupika – Majoka amantaka mkewe Husda ampikie chapatti kwa kuku. Aidha, Ashua ampikia sudi chai na mahamri na kumpelekea kwenye karakana anakochongea vinyago. 
  16. Wazazi wawatafutia wanao wa kiume mke wa kuoa – Kwa mfano, Majoka anamrai Tunu kukubali kuozwa kwa Ngao Junior, mwanawe Majoka lakini Tunu anakataa. 
  17. Wanawake wanaochelewa kuolewa wanakejeliwa na wanajamii wenzao – Kwa mfano, walevi kule Mangweni wanamwimbia Tunu wimbo wa kumkejeli kwa kuchelewa kuolewa ilhali ana elimu ya kutosha. 
  18. Jukumu la mwanamume katika ndoa ni kuikimu familia – Boza anamsuta Sudi kuwa jukumu la mwanamume si kukimbizana na waandamanaji bila kuikimu familia. 
  19. Kuna ndoa za Lazima – Majoka akiwa amezirai anatetea jinsi alivyolazimishwa kumwoa Husda hali iliyomsababishia kulia usiku nzima. (UK. 75)
  20. Umaskini ni chanzo cha kuvunjika kwa ndoa. Kwa mfano , Ashua anamwitisha mumewe sudi talaka akidai kwamba amechokwa kupendwa kimaskini. 
  21. Mapenzi ni wenzo muhimu katika kumchagua mwenzi wa ndoa. Kwa, mfano Majoka anapotaka Tunu aolewe na mwanawe Ngao Junior, Tunu anamwuliza iwapo anaona kuwa hawezi kusubiri akaolewa na mwanamume ampendaye. 
  22. Ndoa imesawiriwa kama jambo, la Lazima kwa yeyote anayetaka kuwa kiongozi. Tunaambiwa kwamba Majoka alilazimishwa kumwoa Husda ili kutimiza wajibu wake katika jamii kama kiongozi. 

Read More
0 Comments

”Hayatapoa…kumewaka na kutateketea tusipouzima moto.Liwalo na liwe!”

21/12/2022

0 Comments

 

​”Hayatapoa…kumewaka na kutateketea tusipouzima moto.Liwalo na liwe!”

a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

  1. Haya ni maneno ya Tunu.
  2. Anamwambia Siti.
  3. Wamo nyumbani mwa akina Tunu.
  4. Ni baada ya Tunu kutaka kujua kwa nini Sudi hajaenda nyumbani kwao kumjulia hali kutokana na kuvamiwa na wahuni ndipo wakajibizana hivi.

b) Bainisha vipengele viwili vya kimtindo vinavyojitokeza katika dondoo hili. (alama 3)

  1. Taswira – Picha moto
  2. Jazanda – Moto (jazanda ya maovu)
  3. Msemo – Liwalo na liwe

c) Tathmini umuhimu wa anayeambiwa maneno haya katika tamthlia. (alama 5)

  1. Anaonyesha ukatili wa Majoka – Anaeleza jinsi Majoka anavyosambaza vikaratasi vya kuwafurusha akina Kombe na Siti kutoka jimboni.
  2. Kuendeleza maudhui ya utu – Anamtembelea Ashua baada ya kutoka gerezani.
  3. Anafunza maadili ya utiifu – Anawapeleka wanawe Sudi nyumbani kwa akina Tunu ili watunzwe na Bi Hashima jinsi alivyokuwa ameagizwa na Tunu.(uk 18)
  4. Kuendeleza maudhui ya mabadiliko – Anabadilika na kuacha kunywa pombe. (uk 58)
  5. Ametumiwa kuchimuza suala la uwajibikaji – Vijana watano wanapouliwa katika kampuni ya Majoka anawafahamisha Tunu na Sudi.
  6. Ametumiwa kubainisha masaibu ya wanyonge – Anasema kwamba tangu jirani yao Sudi aingilie siasa, serikali ya Majoka imekuwa ikiwatisha. (uk 52)

​d) Onyesha jinsi mzungumzaji alivyouzima moto uliokuwa umewaka jimboni Sagamoyo.  (alama 8)

​Mzungumzaji ni Tunu
  1. Majoka anapofunga soko, anawaongoza wachuuzi kuandamana ili kupinga udhalimu huo.
  2. Majoka anapofuja hela za kusafisha soko, anawahutubia waandishi wa habari na kumkashifu. (uk 32)
  3. Majoka anapotumia ajali kumuua Jabali; anapanga kuwaleta wachunguzi wa nje ili kuichunguza ajali hio upya. (uk 35) 
  4. Vijana watano wanapouliwa  katika kampuni ya majoka na majaoka,anaenda hadi ofisini mwa majoka na kumsuta kwa kuwachija watoto wa  wenziwe. Uk 43
  5. Baada ya majoka kutaka kumnyima mamake ,Hashima fidia  baada ya mumewe kufia kwenye kampuni,anasomea uanasheria  ili kujiwezesha kupinga udhalimu kama huu.
  6. Majoka anaponyakua ardhi ya soko la chapakazi kwa lengo la kujenga hoteli,anapinga ujenzi huo kwa kumwambia kuwa hatainjenga hoteli hiyo.-uk45.
  7. Majoka anapofunga  ashua li kumlazimisha  Sudi kumchongea kinyago,anamwambia majoka kuwa lazima watamtoa . Majoka atake au asitake. Uk45.
  8. Majoka alipofunga soko la chapakazi n a kukataa kulifngua , alichoehea raia  kuususia mkutano wa majoka  kwa kuwaaalika mkutano  ambao ungefanyika nje ya lango la soko la chapa kazi, ili,kushurutisha majoka  kuwafungulia soko hilo. Uk 59/86.
  9. Anawazindua raia anapowahutubia  kutowachagua viongozi ambao  wanakiuka haki zao. Akimlenga majoka aliyewaongoza kidhalimu. .uk890.
  10. Asiya anapopika pombe haramu inayowaua  na kuwapofusha  walevi, Tunu anawaeleza walevi madhara haya ilikuwashawishi kuacha kulewa. Uk 63.
  11. Majoka anapofunga soko na kutaa kulifungua  anawaongoza raia kumwondoa mamlakani bila umwagikaji wa damu.

Read More
0 Comments

USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODEL17122022001

17/12/2022

0 Comments

 

​SOMA SHAIRI  KISHA UJIBU MASWALI.

​1. Sidhani ni kichekesho, kesho kuwepo sidhani
Vilivyoko ni vitisho, viwewe na visirani
Mimi kupe kwenye josho, la sumu iso imani
Kesho yangu imeshaliwa.
​2. Kesho yangu imeshaliwa, isibaki hata kitwa
Kwamba hai nitakuwa, kesho na kesho kutwa
Hilo haliwezi kuwa, na wakati limepitwa
Na i wapi kesho yangu?
​3. Sikwambii mtondoo, au ni mtondogoo
Ajapowika jogoo, kesho sipo ng'oo
Hata simu za "haloo", hazinipati "haloo"
Nitaituhumu kesho.
​4. Kesho nitaituhumu, kwa sababu ya hasama 
Hasama ya mahasimu, waliolishana njama
Kutaka kunihujumu, wanizulie nakama 
Itokapi yangu kesho?
​5. Wa kwanza huyu Ukimwi, daima aniotea
Kwa dawa huyu hazimwi, haachi kuturingia
Amekuwa kama zimwi, mtu lisilomjua 
Ati nipangie kesho?!
​6. Nipange yangu matanga, au kujenga nyumba?
Nipange kung'oa nanga, au shairi kuimba?
Nipangeni cha kupanga, biashara za mtumba?
Kesho si ukoo wangu.
​7. Ukimwi nduguze wako, Ebola na Malaria
Kichomi na sekeneko, mno wajifaragua 
Maadamu wangaliko, vipi kesho kuwazia?
Kesho si ndu yangu mwandani.
​8. Mimi napangia leo, maana kesho sijui
Usafiri nifanyao, kwenye vyombo anuwai
Una mikasa kibao, majanga ya kila nui
Salama yangu i wapi?
​9. I wapi salama yangu, huku wapo wa kijicho
Ngaa nipatapo changu, waingiwa mpekecho
Kunipikia majungu, nikikosa changu hicho
Waso nitakia kesho!
10. Kesho wasonitakia, watele kama siafu
Majambazi nasinzia, tapeli na wazinifu
Roho yangu wapania, kunipeleka kwa ufu
Nipewe jina "Hayati"

​MASWALI

​​a. Ujumbe wa shairi hili unakatisha tamaa. Thibitisha. (4)

​Ujumbe wa shairi hili unakatisha tamaa. Thibitisha. (alama 4)
  • Kuna vitisho, viwewe na visirani.
  • Kesho yangu imeshaliwa na hakuna uhakika wa kuifikia.
  • Hapigiwi simu na marafiki
  • Anahujumiwa na watu bila sababu.
  • Kuna magonjwa mbalimbali kama vile Ukimwi na ebola na hayana tiba. 
  • Kuna majambazi na matapeli waliojaa kila mahali. Zozote nne

​b. Hili ni shairi la aina gani? (1)

​Shiari hili ni la Tarbia kwa sababu lina mishororo minne katika kila ubeti.

​c. Andika ubeti wa nne kwa lugha nathari.  (4).

​Mwandishi anaanza kwa kusema kuwa  anaituhumu kesho yake kwa sababu ya uhasama. Anasema uhasama huu unatokana na mahasimu wanaopanga njama ya kumhujumu. Wanataka tu kumsababishia nakama. Mwandishi anamalizia kwa kuuliza kesho yake itatoka wapi na haya mambo yote yanayomzunguka yanaitishia hiyo kesho.

​​d.. Eleza mbinu nne za lugha zilizotumiwa. (4)

  • Isitiari- mimi kupe
  • Kinaya- kesho yangu imeliwa
  • Tanakali ya sauti-  sipo ng'oo
  • Utohozi- haloo
  • Tashihisi- huyu Ukimwi
  • Swali la balagha- Salama yangu i wapi?
  • Tashibihi- kama siafu
  • Nahau-kung'oa nanga

​e. Andika bahari kwa kuzingatia vigezo; (2).
Mizani
Vina

  • Mizani- msuko kwa sababu mizani ya kibwagizo ni michache/ kibwagizo ni kifupi
  • Vina- ukaraguni- kila kipande kinajitegemea kivina​

​f. Onyesho jinsi mshairi alivyotumia idhini yake ya kishairi. (2).

Kufinyanga sarufi- kesho kuwepo sidhani badala ya sidhani kuwepo kesho
Inkisari- iso badala ya isiyo/ Waso badala ya wasio
Tabdila- kitwa badala ya kichwa
zozote mbili

​g. Taja;  (3)
Toni 
Nafsi - neni
Nafsi- nenewa.  

  • Toni – ya kukata tamaa/ kuudhika/ kukosa matumaini/ kuonya
  • Nafsi – neni- mtu asiye na uhakika na kesho yake/ aliyekata tamaa
  • Nafsi- nenewa.- watu kwa jumla/ mahasimu/ wale wanaodhulumu/ wote wanaohujumu

Read More
0 Comments

​KUTIA KWA KULIA NA KUTOA KWA KUSHOTO.

17/12/2022

0 Comments

 

​Kutia kwa kulia na kutoa kwa kushoto.

​I. ELEZA MUKTADHA WA MANENO HAYA. (ALAMA 4)

  • Maneno ya Kenga
  • Anamwambia Majoka
  • Ofisini mwa Majoka
  • Wanaongea kuhusu mshahara wa walimu na wauguzi kuongezwa na Majoka anasema wataiongeza kisha waongeze kodi ili wafanye hesabu ya kutia na kutoandio Kenga akamwambia maneno haya.

​II. FAFANUA MBINU YA LUGHA ILIYOTUMIKA. (ALAMA 2)

  • kinaya- Kutia kwa kulia na kutoa kwa kushoto
  • tanakuzi- kutia na kutoa

​III. FAFANUA SIFA NNE ZA MSEMAJI WA MANENO HAYA. (ALAMA 4)

  • Mshawishi
  • Mpyaro
  • Mwenye vitisho
  • Mwenye hasira
  • Dhalimu
  • Mwoga
  • Fisadi
  • msaliti
  • karagosi
  • nafiki
  • mwoga
  • katili
  • mshauri mbaya

​IV. JADILI MBINU HASI ZA UONGOZI KATIKA TAMTHILIA. (ALAMA 10)

  • Kuua wapinzani. Jabali
  • Kuwapa likizo ndefu. Anataka kuwafurahisha kwani wafanyakazi hawataenda kazini.
  • Kuharamisha maandamano. Ili raia waache kupinga kufungwa kwa soko. 
  • Kufurusha wafadhili wa wapiganiaji haki. Wafadhili wa akina Tunu na Sudi wanatakikana wavunje kambi ili kudhoofisha kifedha.
  • Unafiki/hila/udanganyifu. Kuongeza walimu na wauguzi mshahara lakini anapandisha kodi hivyo hawajafaidika.
  • Kuvunja sheria. Kufuta Kenga kazi kinyume cha katiba kwa kukataa kufyatua risasi kwa raia ambao hawajafanya makosa.
  • Kufukarisha raia. Ili wamtegemee km kufunga soko ambalo ni tegemeo la raia. Ashua anakosa chakula na watoto wakala njaa na akamwendea Majoka msaada. 
  • Kutumia wahuni. Majoka kutumia wahuni kupambana na wapinzani wake km Tunu kuvamiwa na kuvunjwa mguu kwa kupinga soko kufungwa. 
  • Kujaza hofu. Bi Hashima waishi kwa hofu.
  • Kutumia jela. Kufunga Ashua ili mumewe Sudi achongee Majoka kinyago alichokuwa amekataa hapo mbeleni.
  • Kutumia askari. Polisi wanatumia vitoa machozi na risasi ili wasiendelee kupiga soko kufungwa.
  • Kutumia vishawishi na hongo. Tunu na Sudi wanapatiwa kazi katika kiwanda cha Majoka ili wamuunge mkono kisiasa lakini wanakataa. 
  • Kufunga vyombo vya habari. Runinga ya Mzalendo. Kwa kukashifu vitendo vya Majoka kwa kupeperusha maandamano moja kwa moja kupinga kufungwa kwa soko.
  • Tenga tawala. Majoka kutaka kuongea na Tunu na Sudi kando kando, mhuni mmoja kumwambia Tunu kuwa Sudi na Ashua ndio wanawinda  roho yake. 
  • Unasaba. Kuteua binamuye Kenga kuwa mshauri wake mkuu ili iwe rahisi kutekeleza maovu km kuua Jabali.

Read More
0 Comments

Fafanua jinsi Ujenzi wa jamii mpya umeshughulikiwa na mwandishi. (alama 10)

17/12/2022

0 Comments

 

​Fafanua jinsi Ujenzi wa jamii mpya umeshughulikiwa na mwandishi. (alama 10)

  • Usafishaji nafsi- Majoka kuwa tayari kubadilika. Viongozi uacha mabaya na kutenda mema. Uk 84/85
  • Usalama kuimarika. Bwana Kingi kukubali kulinda usalama badala ya kutawanya waandamanaji. Uk89. Uk 90 Kingi kukataa kupiga risasi waliotaka Tunu achaguliwe.
  • Kuchagua viongozi waadilifu- uk 89- Wanasagamoyo kusema hawatakubali kuchagua viongozi wanaowaita wajinga.
  • Kufuata katiba- uk 90 Kingi kusema watu wana mamlaka makubwa kuliko amri za Majoka. Kingi anasema hana ruhusa ya kuvamia watu ambao hawajavunja sharia baada ya Majoka kutaka wapigwe risasi .
  • Kufuata sharia- Majoka anaposema amefuta kazi Kingi kwa kutofuata amri yake ya kupiga waandamanaji risasi, Kingi anamwambia lazima afuate utaratibu  wa kufuta mtu kazi. Uk91
  • Kukubali ukweli- Kingi anakubali uongozi dhalimu umefika mwisho na kuomba msamaha huku akijiunga na umati ilhali Majoka alikataa na kumwiita kunguru. uk 91
  • Kuomba msamaha- Mamapima anaomba msamaha kwa kuuza pomba haramu huku akijua kuwa aliwaponza, aliwapunja, aliwadhuru na alikuwa na tamaa.  uk 92
  • Kuchagua viongozi wanaofaa- kupatia Tunu uongozi hata kama ni mwanamke mradi yuko tayari kuongoza kwa haki.
  • kushirikiana bila kujali maneno ya watu- Tunu na sudiwalishirikiana kupigania haki bila kujali vile watu walisema ulikuwauhusianao wa kimapenzi.
  • kuacha maovu – Mamapima kuapa kuwa hatauza pombe haramu tena inayoua na kupofusha.
zozote 10

Read More
0 Comments

Jadili dhamira ya mwandishi wa Tamthilia ya Kigogo. (alama 10)

17/12/2022

0 Comments

 

​Jadili dhamira ya mwandishi wa Tamthilia ya Kigogo. (alama 10)

  • Kuonyesha umuhimu wa kupinga uongozi mbaya- kuboresha maisha- wananchi wana haki ya kuongozwa vizuri.
  • Kukashifu utepetevu wa viongozi – kutoletea nchi maendeleo yaliyotarajiwa- soko chafu na ukosefu wa kazi.
  • Kuhimiza ushirikiano katika kuondoa uongozi mbaya. Lazima raia waukabili na kuuondoa uongozi wa aina hii.
  • Kufichua uovu wa viongozi- ufisadi, usherati, dhulma, kujilimbikizia mali, ubinafsi, ubadhirifu nk.
  • Kuonyesha madhara  ya ulevi- vifo, upofu, utepetevu nk.
  • Umuhimu wa elimu-kuleta ukombozi- vijana wana mchango mkubwa sana. Km Tunu
  • Kuonyesha athari za umaskini- ukosefu wa kazi na mahitaji ya kimsingi.
  • Kukashifu washauri wabaya wa viongozi – huleta uongozi mbaya.
  • Kuonyesha changamoto za wanaopigania haki- kuumizwa, kuuawa, kutishwa nk.
  • Mwandishi anadhamiria kuonyesha uongozi mbaya na athari zake hasa katika mataifa yanayoendea.Viongozi hutumia mbinu mbalimbali kuongoza zinazowanyanyasa wananchi huku wakijinufaisha wenyewe bila kujali.
  • Kuonyesha kuwa ili kujenga jamii mpya, mapinduzi ni muhimu na ni sharti wananchi wajitolee kwa uzalendo ili kupigania haki zao na usawa na kupinga viongozi wasiofaa.
  • Mwandishi anaonyesha kuwa licha ya changamoto zinazomkumba mwanamke katika jamii, mwanamke ana nafasi muhimu katika uongozi na kuleta maendeleo katika jamii.
zozote 10

Read More
0 Comments

TAMTHILIA YA KIGOGO NI TASWIRA HALISI YA MATATIZO YANAYOKUMBA MATAIFA MENGI BARANI AFRIKA.THIBITISHA

15/12/2022

0 Comments

 

​a)  Tamthilia ya Kigogo ni taswira halisi ya matatizo yanayokumba mataifa mengi barani Afrika.Thibitisha.  (alama 10)

a)  Tamthilia ya Kigogo ni taswira halisi ya matatizo yanayokumba mataifa mengi barani Afrika. Thibitisha.    (alama 10)
  • mauaji ya kiholela-Jabali
  • vitisho kwa wananchi- Chopi
  • unyanyasaji wa wananchi kwa kutozwa kodi ya juu
  • unyakuzi wa ardhi ya umma – soko la Chapakazi
  • kukatiza juhudi za ukombozi-Tunu
  • kutiwa jela bila sababu- Ashua
  • uchafuzi wa mazingira-ukataji wa miti
  • uongozi wa kidikteta- Majoka
  • viongozi kuzawadi vikaragosi wanaounga uongozi wao mkono
  • ukosefu wa ajira kwa waliosoma- Ashua, Tunu
  • viongozi hawataki kutoka uongozini
  • kuendelezwa kwa biashara haramu- Asiya anauza pombe haramu
  • viongozi wanaendeleza ufisadi
  • viongozi kuomba ufadhili kutoka nchi za magharibu kufadhili miradi isiyofaa- uchongaji kinyago                                (zozote 10x1)

​b) Huku ukitoa mifano, angazia nafasi chanya alizopewa mwanamke katika Tamthilia ya Kigogo.   (alama 10)

b) Huku ukitoa mifano, angazia nafasi chanya alizopewa mwanamke katika Tamthilia ya Kigogo.  (alama 10)
  • ni mkombozi- Tunu anatetea haki za wanyonge na hatimaye kuleta mageuzi.
  • Ni mtetezi wa haki- Ashua na Tunu wako katika mstari wa mbele kutetea kazi za wanyonge wanapoenda ofisini mwa Majoka.
  • Mwenye utu- Tunu anamshauri Siti awapeleke watoto wa Sudi kwao.
  • Ni jasiri- Ashua anamkosoa Majoka waziwazi bila uoga.
  • Ni msomi. Ashua ana shahada ya ualimu, Tunu ana shahada ya uanasheria.
  • Ni mwenye heshima- Siti anamsalimu mamake Tunu kwa heshima, Tunu anahutubia wanasagamoyo kwa heshima.
  • Ni mwadilifu- Ashua anakataa kumvunjia Sudi heshima licha ya shinikizo kutoka kwa Majoka.
  • Ni mtiifu- Siti anaposhauriwa awapeleke watoto wa Sudi kwa kina Tunu anafanya hivyo.
  • Ni mwenye msimamo thabiti- Tunu na Ashua wanakataa kushawishiwa na Majoka.
  • Ni mwenye bidii.- Ashua anatia bidii kazini ili amsaidie mumewe kukimu familia.
  • Ni mcha Mungu- Hashima anaamini kuwa Mungu alikuwa amekasirishwa na umwagikaji wa damu Sagamoyo.         (zozote 10x1)       

Read More
0 Comments

‘ Wanaishia kuwa makabeji kwa kudungana sumu ya nyoka.’

15/12/2022

0 Comments

 

‘ Wanaishia kuwa makabeji kwa kudungana sumu ya nyoka.’

‘ Wanaishia kuwa makabeji kwa kudungana sumu ya nyoka.’
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.    (alama 4)
b) Eleza sifa za msemaji wa maneno haya.     ( alama 4)
c) Thibitisha jinsi mwandishi wa tamthilia alivyofaulu kutumia mtindo wa kinaya. (al 8)  
d)    Eleza changamoto zinazoikumba elimu.    (alama 4)

MWONGOZO

‘ Wanaishia kuwa makabeji kwa kudungana sumu ya nyoka.’
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.    (alama 4)
  • Msemaji – Ashua
  • Msemewa – Majoka
  • Mahali  - ofisini mwa Majoka
  • Sababu – majoka alipompendekezea akubali kufunza katika Majoka and Majoka Academy
​b) Eleza sifa za msemaji wa maneno haya.     ( alama 4)
  • Ashua – ni jasiri. Anamkabili Majoka kwa kupaaza sauti ofisini mwake
  • Ni mnyenyekevu. Ananyenyekea mbele ya Majoka ofisini mwake na kumwomba msamaha
  • Ni mwenye heshima. Anakiri kwamba anamheshimu Majoka.
  • Ni mwaminifu.  Anakataa kufanya mapenzi na Majoka kwa kuhofia talaka yake.
  • Ni msomi. Amesomea shahada ya ualimu.
  • Ni mwenye tamaa. Anamwambia Sudi kuwa amechoka kupendwa kimaskini, tama ya mali inamtawala.
  • Ni msaliti. Anasaliti ndoa yake kwa kuomba talaka.                   
  • Ni mwajibikaji. Amewajibika kwa kuwatafutia wanawe chakula.
  • Ni mzalendo. Anakataa kazi anayopewa na Majoka ya kufunza kwa sababu hakutaka kuendeleza ufisadi.
  • Ni mwenye msimamo dhabiti. Anakataa katakata kuhusiana kimapenzi na majoka
 (4x1)
​c) Thibitisha jinsi mwandishi wa tamthilia alivyofaulu kutumia mtindo wa kinaya. (al 8)  
  • Watu wengi wantarajiwa kufika katika uwanja wa ikulu kusherehekea uhuru lakini ni kumi tu wanaofika.
  • Ni kinaya uvumi kuenea kuwa Sudi na Tunu ni wapenzi ilhali wao ni wanamapinduzi.
  • Ni kinaya polisi Sagamoyo kuwatawanya waandamanaji ilhali polisi wanapaswa kulinda na kutetea haki za wananchi.
  • Ni kinaya Ngurumo kudai kuwa tangu soko kufungwa, Sagamoyo ni pazuri zaidi mno na mauzo ni maradufu.
  • Ni kinaya wanasagamoyo kulipa kodi na kitu juu yake ilhali soko halisafishwi.
  • Ni kinaya Majoka kutangaza kufunga soko kwa mwezi mmoja ilhali ni mahali watu wanapata riziki.
  • Ni kinaya Majoka kumpa Asiya kibali cha kuuza pombe haramu ilhali ni kiongozi. Pombe hiyo inasababisha vifo na watu kuwa vipofu.
  • Ni kinaya Ashua kuomba Sudi talaka ilhali walikuwa mume na mke kwa madai kuwa amechoka kupendwa kimaskini.
  • Ni kinaya Kenga kumwacha Majoka ilhali ndiye aliyenufaika na uongozi wake.                                                                   (8x1)
d) Eleza changamoto zinazoikumba elimu.  (alama 4)
  • Ukosefu wa ajira kwa waliosoma, mfano Tunu na Ashua
  • Matumizi ya dawa za kulevya- wanafunzi katika shule ya Majoka wanadungana sumu ya nyoka.
  • Wivu- husda anamuonea kijicho Ashua kwa kuwa amesoma licha ya kuwa yeye ana kisomo cha msingi.
  • Ukiukaji wa haji-  Tunu na Sudi wanapigania haki za wanafunzi wenzao chuoni
  • Mtazamo hasi kuhusu walimu- Ngurumo hakuwa na uhusiano mwema na mwalimu wake wa somo la Historia.
  • Migomo- walimu wanagoma kila wakati.
  • Mtazamo hasi  kwa walioelimika-  mfano Majoka na Kenga wanadharau shahada ya udaktari ya Tunu.
  • Wanafunzi kuishia kuwa ovyo- wanafunzi wa shule ya Majoka and Majoka Academy wanaishia kuwa makabeji kwa kudungana sumu ya nyoka.
  • Ufisadi. Majoka anamwambia Ashua kuwa angekuwa akifunza katika shule mojawapo ya kifahari.

Read More
0 Comments

​WA KUREJELEA TAMTHLIA YA 'KIGOGO YA PAULINE KEA, ONYESHA JINSI AMBAVYO VIONGOZI WENGI KATIKA NCHI ZA KIAFRIKA WAMEJAWA NA TAMAA.

14/12/2022

0 Comments

 

​wa kurejelea tamthlia ya 'Kigogo ya Pauline Kea, onyesha jinsi ambavyo viongozi wengi katika nchi za kiafrika wamejawa na tamaa.         (alama 20)

mwongozo

Tamaa ya kupata sanamu/ Majoka anataka Sudi amtengenezee sanA
  1. Tamaa ya kupata kodi. Majoka anawatoza kodi wafanyibiashara wa soko la Chapakazi kwa manufaa yao.
  2. Tamaa ya shule zao kufunzwa na walimu waliofuzu vyuoni. Majoka anamrai Ashua afunze katika shule zake.
  3. Tamaa ya kuungwa.  Majoka anapata uungwaji mkono kupitia watu kama Ngurumo, Asiya na Boza -
  4. Anawapa hongo ili wamuunge mkono.
  5. Tamaa ya kupewa sifa lufufu. Kwa mfano Majoka lazima atangazwe katika vyombo vya habari.
  6. Tamaa ya kutafutia wanao wachumba. Majoka anamtaka Tunu aolewe na mwanawe Ngao Jur.
  7. Tamaa ya mapenzi -  Majoka ana tamaa ya kupendwa na Ashua.
  8. Tamaa ya kujenga nyumba za kifahari. Majoka anatamani kujenga hoteli ya kifahari katika soko la Chapakazi.
  9. Tamaa ya usalama -  Majoka ana walinzi wengi.
  10. Starehe na anasa. Majoka ana tamaa ya burudani. Anaenda kuogelea katika hoteli ya‘ Majoka and Majoka  resort’
  11. Tamaa ya viongozi kurithisha jamaa zao uongozi.

Read More
0 Comments

Uliona nini kwa huyo zebe wako ? Eti mapenzi!

14/12/2022

0 Comments

 

​Uliona nini kwa huyo zebe wako ? Eti mapenzi!

Uliona nini kwa huyo zebe wako ? Eti mapenzi!
a. Eleza muktadha wa dondoo. (al. 4)
b. Andika mbinu za lugha zinazojitokeza kwenye dondoo hili (al. 4)
c. Taja hulka za mnenaji unajitokeza katika dondoo. (al. 2)
d. Mwanamke ni kiumbe wa kukandamizwa. Thibitisha kauli hii ukirekjelea tamthilia. (al. 10)

​MWONGOZO

​i) – Maneno ya Majoka
- Anamwambia Ashua
- Ofisini mwa Majoka
- Ni baada ya Ashua kumkataa Majoka Kimapenzi alipokwenda kutaka msaada kwake                   1 x 4   =  4
​ii) Mbinu – Swali la balagha – uliona nini kwa huyo zebe wako?       (al 2 )
- Nidaa – Eti mapenzi!       (al 2 )
- Kutaja alama 1
- Mfano alama 1
​iii) Hulka za Majoka
- Dharau/ bezo – Eti mapenzi!
- Mpyaro – zebe ( mjinga / mpumbavu)    1 x 2 = 2
1x 2  = 2 Mwalimu akadirie
iv) Ukandamizaji wa mwanamke 
  • kupigwa:  Ashua akiwa gerezani anapigwa na askari
  •  kubezwa / kukejeliwa:  Tunu anakejeliwa na Ngurumo na walevi wengine
  • Chombo cha mapenzi.  Majoka anamtaka Ashuakimapenzi anapokwenda kumwomba msaada.
  • Kijakazi nyumbani.  Majoka anamtuma chopi kumuagiza mkewe kumpikia kuku na nyama na kumuokea chapatti
  • Kutusiwa.  Boza anamwambia Sudi kuwa asifikiri kuwa yeye anauza nyong’a kama Tunu wake.
  • Kufungwa.  Ashua anafungwa na Majoka
  • Kunyimwa kura/uongozi.  Nurumo anamwambia Tunu kuwa kama hampi kura Majoka ni heri ampe paka wake.  Majoka lakini si mwanamke Tunu.
  • Kunyimwa ajira.  Licha ya Ashua kufuzu taaluma ya ualimu, hakuajiriwa na serikali.  Anaishia kuchuuza maembe sokoni la chapakazi.
  • Kuozwa bila hiari. Majoka nataka kumwoza Tunu kwa mwanawe Ngao Junior bila hiari yake.
  • Kunyimwa fidia. Majoka alitaka kumnyima Hashima fidia baada ya kifo cha mumewe

Read More
0 Comments

“Huku ni Sagamoyo, naomba kukukumbusha kuwa serikali na katiba ni mambo mawili tofauti kabisa!”

14/12/2022

0 Comments

 

​“Huku ni Sagamoyo, naomba kukukumbusha kuwa serikali na katiba ni mambo mawili tofauti kabisa!”

​a) Eleza Mukutadha wa mambo haya.   (alama 4)

​i. Msemaji: Ngurumo
ii. Msemewa: Tunu
iii. Mahali: Mangweni (kwa mamapima/Asiaya)
iv. Kiini: Sudi na Tunu walipotaka kujua sababu ya Mamapima kudai kuwa ana kibali cha kuuza pombe haramu.  (4x1=4)

​b) Msemaji ana umuhimu gani katika serikali inayotajwa.    (alama 6)

​i. Ngurumo ni kielelezo cha namna vijana walevi wanavyotumiwa na viongozi kuendeleza maovu katika jamii. Alitumiwa kumshambulia Tunu na kumuumiza.
ii. Anadhihirisha namna vijana wanavyotekwa akili kwa njia rahisi kwa malipo kichele (fedha kidogo)
iii. Viongozi wenye ubinafsi wanajali maslahi yao tu na kutumia vijana ambao ni nguvukazi ya taifa vibaya. 
iv. Anaonyesha kuwa watawala waovu hawawezi kuendeleza utawala wa mabavu bila kutumiaraia wengine.
v. Kifo cha Ngurumo kinadhihirisha ukatili wa Majoka ambaye hakuonyesha chembe cha huruma alipojulishwa juu ya kifo cha Ngurumo.
vi. Anadhihirisha athari mbaya za ulevi zinavyoambatana na tabia zingine mbaya za upyaro na uzinzi.   (6x1=6)

​c) Fafanua kasoro zozote kumi za serikali inayorejelewa.   (alama 10)

  1. Viongozi ni wabinafsi: Viongozi katika serikali hii wanajinufaisha na kufaidi matunda ya uhuru huku wananchi wa Sagamoyo wakiumia. Majoka anaamua kufunga soko la Chapakazi, ambalo ni tegemeo la Wanasagamoyo; badala yake ajenge hoteli yake ya kifahari.
  2. Viongozi wanaendeleza ufisadi. Majoka anamtengea mshauri wake (Kenga) kiwanja katika soko hilo.
  3. Ukiukaji wa katiba: Uongozi unakiuka katiba ya nchi, hali ambayo inaelekea ukosefu wa demokrasia. Mwandish anaonyesha suala hili wakati Ngurumo anamtahadharisha Tunu kuwa serikali ya Sagamoyo na katiba ni mambo mawili tofauti kabisa; hivyo asishangae kuona pombe haramu ikitengenezwa na kuuzwa wakati sharia zinazuia kufanya hivyo.
  4. Uonzozi wa Majoka hauthamini utu wa kibinadamu. Utawala wake unaua vijana watano wa kampuni yake waliokuwa wameandamana kudai maslahi yao.
  5. Uongozi wa Majoka hauheshimu uhuru wa vyombo vya habari kama vile runinga, magazeti na mitandao ya kijamii. Baada ya runinga ya Mzalendo kurusha mubashara (live) maandamano yaliyoongozwa na Tunu Majoka anaamuru runinga hiyo ichukuliwe hatua ambazo aghalabu ni kufungiwa.
  6. Pana matumizi mabaya ya vyombo dola. Askari wanawapiga watu baada ya kutiwa korokoroni. Kwa mfano, baada ya Ashua kuwekwa nguvuni Sudi anaambiwa na Chopi kuwa anaona atapata fursa nyingine ya kumfanyia uhayawani huenda si mara moja au mbili.
  7. Uharibifu wa mazingira:  Kigogo anaruhusu biashara ya kukata miti. Hii inasababisha Sagamoyo ikumbwe na ukame na njaa. 
  8. Vitisho kwa raia. Uatawala wa Majoka unatoa vitisho kwa raia ambao wanaonekana kupinga utawala wake. Kwa mfano vijikaratasi ambavyo vilitaka jamii ya kina Kombe na Siti ihame. 
  9. Hakuna uhuru wa kuandamana kudai haki. Vijana watano wanauawa wanapokuwa kwenye maandamano. 
  10. Viongozi wanaanzisha miradi isiyofaidi wananchi kivyovyote vile. Kwa mfano kampuni ya kuzalisha sumu ya nyoka na mradi wa kuchonga vinyago.
  11. Sekta ya elimu imepuuzwa. Wanafunzi katika shule ya Majoka academy hawafuzu, wanaishia kuwa makabeji.
  12. Wanasagamoyo wanalipishwa kodi na kitu juu.   (10x1=10)

Read More
0 Comments

“Huwezi kuyang’amua kwa kuwa umeyafumbia macho.  Hujaibambua ngozi yako ya zamani”.

14/12/2022

0 Comments

 

​“Huwezi kuyang’amua kwa kuwa umeyafumbia macho.  Hujaibambua ngozi yako ya zamani”.

​(a) Eleza muktadha wa dondoo.   (alama 4)

  • ​Msemaji: Babu
  • Msemewa: Majoka
  • Mahali: Katika chumba cha wagonjwa (hospitalini alimolazwa Majoka)
  • Kiini: Katika ndoto, Majoka alitaka kujua kwa Babu yake kama watu wanamhukumu.  Babu alimwambia hakimu wake ni yeye mwenyewe na Majoka akaonekana kutong’amua maneno hayo.                (4 x 1 = 4)

​(b) Eleza sifa mbili za kimtindo zilizotumika katika dondoo hili.  (alama 4)

  1. Jazanda: “Hujaibambua ngozi yako ya zamani” kumaanisha hajaacha tabia / hulka yake ya zamani. Ngozi inarejelea tabia au sifa za mtu. 
  2. Nahau: Fumba macho; kujifanya haoni/kujitia hamnazo/kupuuz jambo.  (2 x 2=4)

​(c) Kwa hoja sifa, fafanua umuhimu wa msemaji wa maneno haya.     (alama 6)

Msemaji ni Babu
  1. Kupitia mazungumzo haya, udhalimu aliotekeleza Majoka unaonekana kupitia kwa hukumu ya ndani kabisa ya nafsi yake.
  2. Ni kielelezo cha wazee wenye hekima na Busara kupitia kwa ushauri wake kwa Majoka. 
  3. Anaibua uongozi mbaya wa Majoka kwa kudhihirisha jinsi alivyo rubani aliyeacha usukani kwa mikono ya watu wengine.
  4. Babu anafunulia Majoka kuwa wakati wa Mabadiliko umefika na ni sharti Majoka akumbatie.
  5. Ni kielelezo cha maadili mema katika jamili anapouusia Majoka abadili njia zake, atende wema badala ya uovu kwani wema hauozi.
  6. Anaendeleza maudhui ya utamaduni kwani alikuwa amevalia maleba ya  kitamaduni.
  7. Anabainisha kutowajibika kwa Majoka kimaendeleo na kwamba ameshindwa na    uongozi ndio maana anawaachia marubani wengine kukiendesha chombo.
  8. Anaibua ukatili na udhalimu wa majoka, hivi kwamba amewaua watu wengi sana kiwango cha damu kuwa kama bahari.
Tathmini hoja nyinginezo za mtahiniwa. (Zozote 6 x 1 = 6)

​(d) Thibitisha vile mrejelewa anavyofumbia macho hali inayomkabili.    (alama 6)

[Hali inayomkabili Majoka ni kuzinduka kwa wanasagamoyo kudai haki zao kutokana na uongozi mbaya wa Majoka. Sasa anaona yote aliyoyafumbia macho ndio yanamhukumu.]
  1. Anafunga soko la Chapakazi linalotegemewa na wengi bila kujali mateso wanasagamoyo wanapitia.
  2. Anaua wapinzani wake wa kisiasa kwa mapuuza ya matokeo yake ya baadaye. (Jabali), anapanga mauaji ya Tunu, akaishia kuvunjwa mguu.
  3. Anafungulia ukataji wa miti ovyo bila kujali madhara yake kwa mazingira.
  4. Anafungua kampuni ya kuzalisha sumu ya (dawa za kulevya) na anajivunia sana jambo huku akipuuza madhara yake kwa jamii.
  5. Wanafunzi katika shule yake hawafuzu, wnaishia kuwa makabeji kwa kudungana sumu ya nyoka. Majoka haonekani kushtuliwa na jambo hili.
  6. Anakubali kufuata ushauri mbaya wa Kenga wa kutia Ashua gerezani bila kosa. Anajifanya haoni kuwa hii ni dhuluma kwa wanyonge. 
  7. Anapuuza katiba ya nchi na kuendelea kuongoza Sagamoyo anavyotaka. “Huku ni Sagamoyo,…. Serikali na katiba ni mambo mawili tofauti kabisa..”
  8. Anampa Asiya (Mamapima) kibali cha kuuza pombe haramu bila kujali kuwa pombe hiyo inawaponza na kuwaua vijana.
  9. Hajali utu wa kibinadamu. Anasema Ngurumo ni kimba tu, azikwe juu yaw engine.
  10. Anawatukana wanasagamoyo “Wajinga” bila kujali nguvu za umati dhidi yake mtu mmoja.
[Tathmini hoja nyinginezo za mtahiniwa. Zozote 6 x 1 = 6]

Read More
0 Comments

“Tuacheni kufumbatia maji kama jiwe. Sagamoyo inahitaji mabadiliko ,damu nyepesi ili kuufungua ukurasa mpya.”

13/12/2022

0 Comments

 

​“Tuacheni kufumbatia maji kama jiwe. Sagamoyo inahitaji mabadiliko ,damu nyepesi ili kuufungua ukurasa mpya.”

a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
b) Kwa kutoa mifano taja vipengele vine vya kimtindo vinavyojitokeza katika dondoo hili. (alama  4) 
c) Fafanua umuhimu wa mandhari husika katika kuijenga tamthilia.    (alama 5)
d) Kwa nini Sagamoyo inahitaji mabadiliko (alama 5)
e) Eleza jinsi mwandishi alivyotumia taswira. (alama 2)

MWONGOZO

“Tuachenikufumbatiamajikamajiwe. Sagamoyoinahitajimabadiliko ,damunyepesiilikuufunguaukurasampya.”
a) Elezamuktadhawadondoohili. (alama 4)

Maneno ya SudikwaNgurumo, Boza na Waleviwengine.
Walikuwamangweni .
Walikuwawameendakuwaalikawaendekwenyelangokuu la chapakazi
b) Kwa kutoamifanotajavipengelevinnevyakimtindovinavyojitokezakatikadondoohili. (alama  4)
Misemo- damunyepesi
Tashbihi-kufumbatiamajikamajiwe.
Jazanda –damunyepesi/ kufunguaukurasampya.
Taswira-kufumbatiamaji/ kufunguaukurasampya.
c) Fafanuaumuhimuwamandharihusikakatikakuijengatamthilia.   (alama 5)
Sifazawahusika / mhusikayeyotekwenyemandharihusika.
Maudhuiyanajitokeza
Mtirirkowavitushi/ ploti.
Ufaafuwaanwani.
Kielelezo cha mahali/ eneohusika.

​d) Kwa ninisagamoyoinahitajimabadiliko. (alama 5)

i) Sagamoyoimekumbwanamatatizomengikama vile mauaji ya kiholelamfanojabali, ngurum, vijanawatano.
ii) Kunyakuliwakwaardhi na Majoka na Kenga.
iii) Ukatili/ ukosefuwa utu- Majokaanaamrishawatuwapigwerisasibilakujali.
iv) Jimbohlilinaelimumbovu-inawalemazabadala ya kuwaandaawawewazalendowakujenganchi.
v) Ufisadi- wafanyakazikutozwakodi.
vi) Ukatajiwamtiunaosababishaukame na uhaba wa maji na Majoka.
vii) Utawalawakimila au udikteta- Majokaanatakaaendeleekutawalaingawaurubaniumemshinda na amezoroteshanchi.
viii) Mazingiramachauhasaeneo la soko.
ix) Matumizimabaya ya vyombovyadola.
x) Ukosefuwakazi kwa vijanakama vile: Ashua na Tunulicha ya kuwa na kisomo.
xi) Gharama ya maishakupandahasabei ya chakulakwenyevioski. 

e) Elezajinsimwandishialivyotumiataswira. (alama 2)

Taswiraoni-kuufunguaukurasampya
Taswiramguso-kufumbatiamajikamajiwe.

Read More
0 Comments

​ULIONA NINI KWA HUYO ZEBE WAKO ? ETI MAPENZI!

23/6/2021

0 Comments

 

​TAMTHILIA YA KIGOGO 

​Uliona nini kwa huyo zebe wako ? Eti mapenzi!

a. Eleza muktadha wa dondoo. (al. 4)
b. Andika mbinu za lugha zinazojitokeza kwenye dondoo hili (al. 4)
c. Taja hulka za mnenaji unajitokeza katika dondoo. (al. 2)
d. Mwanamke ni kiumbe wa kukandamizwa. Thibitisha kauli hii ukirekjelea tamthilia. (al. 10)

​wa kurejelea tamthlia ya 'Kigogo ya Pauline Kea, onyesha jinsi ambavyo viongozi wengi katika nchi za kiafrika wamejawa na tamaa

Maneno ya Majoka
  1. Anamwambia Ashua
  2. Ofisini mwa Majoka
  3. Ni baada ya Ashua kumkataa Majoka Kimapenzi alipokwenda kutaka msaada kwake                                                     
Mbinu – Swali la balagha – uliona nini kwa huyo zebe wako?  
  1. Nidaa – Eti mapenzi! 
  2. Kutaja alama 1
  3. Mfano alama 1
Hulka za Majoka
  • Dharau/ bezo – Eti mapenzi!
  • Mpyaro – zebe ( mjinga / mpumbavu)
  • Mwalimu akadirie
Ukandamizaji wa mwanamke 
  • kupigwa:  Ashua akiwa gerezani anapigwa na askari
  • kubezwa / kukejeliwa:  Tunu anakejeliwa na Ngurumo na walevi wengine
  • Chombo cha mapenzi.  Majoka anamtaka Ashuakimapenzi anapokwenda kumwomba msaada.
  • Kijakazi nyumbani.  Majoka anamtuma chopi kumuagiza mkewe kumpikia kuku na nyama na kumuokea chapatti
  • Kutusiwa.  Boza anamwambia Sudi kuwa asifikiri kuwa yeye anauza nyong’a kama Tunu wake.
  • Kufungwa.  Ashua anafungwa na Majoka
  • Kunyimwa kura/uongozi.  Nurumo anamwambia Tunu kuwa kama hampi kura Majoka ni heri ampe paka wake.  Majoka lakini si mwanamke Tunu.
  • Kunyimwa ajira.  Licha ya Ashua kufuzu taaluma ya ualimu, hakuajiriwa na serikali.  Anaishia kuchuuza maembe sokoni la chapakazi.
  • Kuozwa bila hiari. Majoka nataka kumwoza Tunu kwa mwanawe Ngao Junior bila hiari yake.
  • Kunyimwa fidia. Majoka alitaka kumnyima Hashima fidia baada ya kifo cha mumewe
Tamaa ya kupata sanamu/ Majoka anataka Sudi amtengenezee sana
  • Tamaa ya kupata kodi. Majoka anawatoza kodi wafanyibiashara wa soko la Chapakazi kwa manufaa yao.
  • Tamaa ya shule zao kufunzwa na walimu waliofuzu vyuoni. Majoka anamrai Ashua afunze katika shule zake.
  • Tamaa ya kuungwa.  Majoka anapata uungwaji mkono kupitia watu kama Ngurumo, Asiya na Boza -
  • Anawapa hongo ili wamuunge mkono.
  • Tamaa ya kupewa sifa lufufu. Kwa mfano Majoka lazima atangazwe katika vyombo vya habari.
  • Tamaa ya kutafutia wanao wachumba. Majoka anamtaka Tunu aolewe na mwanawe Ngao Jur.
  • Tamaa ya mapenzi -  Majoka ana tamaa ya kupendwa na Ashua.
  • Tamaa ya kujenga nyumba za kifahari. Majoka anatamani kujenga hoteli ya kifahari katika soko la Chapakazi.
  • Tamaa ya usalama -  Majoka ana walinzi wengi.
  • Starehe na anasa. Majoka ana tamaa ya burudani. Anaenda kuogelea katika hoteli ya‘ Majoka and Majoka  resort’
  • Tamaa ya viongozi kurithisha jamaa zao uongozi.

Read More
0 Comments

Fafanua jalada la tamthilia kigogo

13/6/2020

0 Comments

 

Fafanua jalada la tamthilia kigogo

0 Comments

"Wananchi katika mataifa ya Afrika hukumbwa na matatizo ya viongozi wanafiki."Thibitisha kauli hii kwa kutolea mifano kutoka tamthilia ya kigogo.

13/6/2020

2 Comments

 

"Wananchi katika mataifa ya Afrika hukumbwa na matatizo ya viongozi wanafiki."Thibitisha kauli hii kwa kutolea mifano kutoka tamthilia ya kigogo.

2 Comments

Mwandishi wa kigogo amewajenga wanawake kwa njia hasi na chanya.Jadili kauli hii kwa kutolea mifano kutoka tamthilia

13/6/2020

0 Comments

 

Mwandishi wa kigogo amewajenga wanawake kwa njia hasi na chanya.Jadili kauli hii kwa kutolea mifano kutoka tamthilia

0 Comments

Jadili ufaafu wa anwani"kigogo"katika tamthilia ya kigogo.

13/6/2020

2 Comments

 

Jadili ufaafu wa anwani"kigogo"katika tamthilia ya kigogo.

2 Comments

Jadili jinsi maudhui  ya uzalendo yamejitokeza katika tamthilia ya Kigogo

13/6/2020

3 Comments

 

Jadili jinsi maudhui ya uzalendo yamejitokeza katika tamthilia ya Kigogo

3 Comments

"Maandamano na migomo ni tatizo sugu katika mataifa yanayoendeleaa."Kwakurejelea tamthilia ya kigogo,eleza chanzo  na athari za maandamano na migomo.

13/6/2020

1 Comment

 

"Maandamano na migomo ni tatizo sugu katika mataifa yanayoendeleaa."Kwakurejelea tamthilia ya kigogo,eleza chanzo na athari za maandamano na migomo.

1 Comment
<<Previous
    KIGOGO

    author

    M.A NYAMOTI

    B.ed Science

    archives

    Archives

    February 2023
    December 2022
    June 2021
    June 2020

    category

    Categories

    All
    MAUDHUI
    Mbinu Za Lugha Na Sanaa
    Mwongozo Wa Kigogo
    SWALI NA JIBU
    UFAAFU WA JALANDA
    WAHUSIKA NA SIFA ZAO

    rss feeds

    RSS Feed


    HIGH SCHOOL EXAMINATIONS

    open

    ENGLISH LITERATURE BOOKS & SETBOOKS

    open

    KCSE KISWAHILI SETBOOKS

    open

    Geography Form 1 Notes and Other Resources

    open

    KCSE PAST PAPERS BY SUBJECT 1989 - LAST YEAR

    open

    Geography Form 2 Notes and Other Resources

    open

    KCSE Past Papers, Marking Schemes and Reports

    open

    BIOLOGY FORM 1 NOTES

    open

    ALL SECONDARY RESOURCES (EXAMINATIONS, NOTES, TUTORIALS AND REPORTS)

    open

    PRIMARY SCHOOL RESOURCES 8-4-4

    open

    KCPE Past Papers, Marking Schemes and Reports

    open

    STANDARD 8 CLASSROOM RESOURCES

    open

    PRIMARY SCHOOL RESOURCES CBC

    open

    COLLEGE RESOURCES

    open

    NAIROBI UNIVERSITY STUDENTS RESOURCES

    open

    KNEC Past Papers For College and other Resources

    open

    FREE NOVELS

    open
Click to set custom HTML


Primary Resources
  • K.C.P.E Past Papers
  • ​Pri - Primary 1 Level
  • Pri  - Primary 2 Level
  • Grade 1
  • Grade 2
  • Grade 3
  • Grade 4
  • Standard 5
  • Standard 6
  • Standard 7
  • Standard 8
  • English
  • Kiswahili
  • Social Studies
  • Science
  • Mathematics
  • Kenya Sign Language
  • I.R.E
  • ​H.R.E
  • Notes
  • Termly Questions
  • Mocks
  • K.C.P.E Past Papers
College Resources
  • E.C.D.E
  • P.T.E
  • D.T.E
  • Technical Diploma
  • Technical Certificate
  • Business Diploma
  • Business Certificate
  • Higher Diploma
  • K.A.S.N.E.B Resources
  • K.M.T.C Resources
  • Varsity Resources
Secondary Resources
  • K.C.S.E Past Papers
  • Form 1
  • Form 2
  • Form 3
  • Form 4
  • Term 1
  • Term 2
  • Term 3
  • English
  • Geography
  • History
  • C.R.E
  • I.R.E
  • ​H.R.E
  • Home Science
  • Computer Studies
  • Business Studies
  • Agriculture
  • Chemistry
  • Biology
  • Physics
  • Mathematics ALT A
  • Mathematics ALT B
  • Kiswahili
  • French
  • Germany
  • Arabic
  • Aviation
  • Art & Design
  • Drawing & Design
  • Building & Construction
  • Metal Works
  • Wood Work
  • Music
  • Kenya Sign Language
  • Electricity
Other Useful Links
  • Academic Environment
  • How its Done
  • News and Opinions
  • Manyam Franchise Support
  • About
  • SITEMAP
  • FOCUS A365 SERIES
  • Membership Details (KCPE/KCSE)
  • Secondary Mocks
  • SYLLABUS
Contact Us
Manyam Franchise
P.O Box 1189 - 40200 Kisii
Tel: 0728 450 424
Tel: 0738 619 279
Tel: 0763 450 425
E-mail - sales@manyamfranchise.com
  • Start
    • Help & Support >
      • About Us
    • Academic Environment
    • KNOWLEDGE CENTRE
    • How its Done
    • NICHE PAGES >
      • The Constitution of Kenya, 2010
      • Atika School Short Stories for 7-12 Years Learners
      • KNEC Portal
      • ZERAKI HELP AND SUPPORT
      • KNEC KCSE PROJECT INSTRUCTIONS
      • JOBS IN KENYA AND ABROAD FOR KENYANS AND BEYOND
  • MEMBERS PORTAL
  • BLOGS
    • QUESTIONS & ANSWERS >
      • SECONDARY >
        • LANGUAGES >
          • Secondary English Questions and Answers
        • TECHNICALS >
          • COMPUTER STUDIES >
            • KCSE Computer Studies Questions and Answers: Comprehensive Analysis and Resources
            • kcse computer studies paper 2 AND 3 Questions & Answers
          • BUSINESS STUDIES QUESTIONS & ANSWERS
          • KCSE AGRICULTURE TOPICAL QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCSE HOME SCIENCE DIRECT QUESTIONS AND ANSWERS
        • SCIENCES >
          • KCSE Mathematics Topical Questions
          • KCSE Biology Topical Questions and Answers
          • CHEMISTRY TOPICAL QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCSE Physics Topical Questions
          • KCSE physics Practical Sample Quiz
        • HUMANITIES >
          • ATIKA SCHOOL - KCSE CRE Questions and Answers
          • ISLAMIC RELIGIOUS EDUCATION (IRE) QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCSE History Topical Questions and Answers
          • GEOGRAPHY TOPICAL QUESTIONS AND ANSWERS
      • PRIMARY >
        • Standard 4-8 Mathematics Topical Questions from Mocks and KCPE
        • Std 6 Mathematics Notes
    • TUTORIALS >
      • SECONDARY >
        • SCIENCES >
          • FOCUS MATHEMATICS TUTORIALS AND EXAMS FREE
          • KCSE BIOLOGY NOTES
          • FREE KCSE CHEMISTRY NOTES
          • KCSE PHYSICS NOTES, AUDIOVISUALS AND MORE
        • LANGUAGES >
          • ENGLISH >
            • FATHER OF NATIONS STUDY GUIDE
            • A GUIDE TO SILENT SONG AND OTHER STORIES
            • English KCSE Set Books
            • ENGLISH POETRY QUESTIONS WITH ANSWERS FOR K.C.S.E CANDIDATES
            • KCSE English Grammar: A Comprehensive Guide for Students
          • KISWAHILI >
            • Bembea ya Maisha
            • CHOZI LA HERI - MWONGOZO
            • KIGOGO - MWONGOZO
            • MASWALI NA MAJIBU YA TUMBO LISILOSHIBA
            • USHAIRI MASWALI NA MAJIBU
            • KCSE Kiswahili Fasihi
        • TECHNICALS >
          • COMPUTER STUDIES NOTES LATEST
          • HOME SCIENCE NOTES
          • KCSE BUSINESS STUDIES NOTES
          • KCSE AGRICULTURE NOTES, SYLLABUS, QUESTIONS, ANSWERS, SCHEMES OF WORK AND OTHERS
        • HUMANITIES >
          • KCSE History Notes Form 1 to 4
          • FREE KCSE CRE NOTES
          • KCSE GEOGRAPHY NOTES
          • IRE NOTES, AUDIOVISUAL, QUESTIONS AND ANSWERS
      • PRIMARY >
        • STANDARD 4: SOCIAL STUDIES
        • NOTES >
          • KISWAHILI
          • SOCIAL STUDIES
        • EXAMINATIONS
        • DecaTurbo Online Series Examinations
        • KCPE Mathematics Notes
        • KCPE and Primary Level Compositions
      • Other Supportive Documents >
        • SYLLABUS >
          • Primary 8-4-4 based Syllabus, Objectives and Lessons
          • Primary Mathematics Syllabus
        • MASOMO VIDEOS
    • EXAMINATIONS >
      • MOCKS AND JOINT EXAMS >
        • FORM 1 QUESTION PAPERS, ANSWERS AND MARKING SCHEMES COLLECTIONS
        • FORM 2 QUESTION PAPERS, ANSWERS AND MARKING SCHEMES COLLECTIONS
        • FORM 3 EXAMINATIONS, QUESTION PAPERS AND ANSWERS
        • FORM 4 MOCKS PAST EXAMS BY REGION
        • TOP SECONDARY EXAMS ALL SUBJECTS
      • KPSEA NATIONAL EXAMS
      • KCPE >
        • KCPE PAST PAPERS AND ANSWERS >
          • KCPE 2020 RESULTS, REPORTS, QUESTIONS AND ANSWERS
          • KCPE PAST PAPERS 2019 REPORTS, RESULTS, QUESTIONS AND ANSWERS
        • KCPE PAST PAPERS PER SUBJECT
      • KCSE >
        • KCSE PAST PAPERS BY SUBJECT
        • KNEC KCSE PAST PAPERS, MARKING SCHEMES, QUESTIONS & ANSWERS
        • Free KCSE Past Papers Mathematics
        • Free KCSE Biology Questions and Answers
  • OUR PRODUCTS
    • All Categories >
      • MORE PRODUCTS >
        • SECONDARY CRE NOTES
        • COURSE BOOKS
        • KCSE KISWAHILI SETBOOKS
        • Backed Up Files and Archives
        • FREE DOCUMENTS
        • PRIMARY 8-4-4 BASED RESOURCES
        • STANDARD 8 RESOURCES
        • HIGH SCHOOL RESOURCES >
          • Biology Paper 3 Exams
          • Secondary Examinations
        • PRIMARY CBC BASED RESOURCES
        • COLLEGE & VARSITY RESOURCES
      • PRIMARY RESOURCES CBC
      • PRIMARY RESOURCES 8-4-4
      • SECONDARY RESOURCES
      • NOTES & TUTORIALS
      • COLLEGE RESOURCES
      • NOVELS and OTHER BOOKS
    • CURRICULUM >
      • NEW CURRICULUM DESIGNS >
        • PRIMARY >
          • PRE PRIMARY ONE CURRICULUM WITH SYLLABUS
          • PRE PRIMARY TWO CURRICULUM WITH SYLLABUS
        • SECONDARY >
          • KNEC KCSE SYLLABUS AND COURSE OUTLINES
        • COLLEGE >
          • Regulations for the TIVET Craft and Diploma Business Examinations
    • HIGH INSTITUTIONS >
      • EXAMINATIONS >
        • College and Varsity Past Papers online
      • TUTORIALS >
        • COLLEGE AND UNIVERSITY NOTES AND TUTORIALS