Maswali na Majibu KCSE Kiswahili
Ufahamu | Ufupisho | Isimu Jamii | Insha | Utumizi wa Lugha
Hakikisha kuwa insha yako ina mpangilio mzuri na mtiririko unaofuata hoja kuu.Kuandika insha ni mchakato wa kutumia maneno na sentensi kuwasilisha wazo, mtazamo, au maoni juu ya suala fulani. Hapa kuna hatua muhimu za kuandika insha:
0 Comments
Majibu
SWALI LA 1. -Mwanafunzi aandike insha yenye kuhusu mazungumzo au majibizano kati ya wahusika hawa watatu -Insha ifuate mtindo wa mchezo wa kuiguza - Azingatie kisa cha utovu wa nidhamu kama vile kupigana na mwanafunzi mwenzake, kuchelewa, kutovaa sare za shule n.k - Mwanafunzi atumie maneno mia nne (400). Asiyefikia maneno mia nne aondolewe maki 2 yaani 2u - Asipozingatia sura aondilewe maki 4 yaani 4s. SWALI LA 2
Faida ya kuelimisha motto wa kike
Maana ya methali SWALI LA 4 -Mwanafunzi atunge kisa ambacho kitaonyesha kuwa anajuta baada ya kutozingatia mawaidha -aliyopewa hapo awali -Mwanafunzi asiyemalizia kwa maneno haya awekwe katika kiwango cha D (alama3) -Akiongeza au kupunguza maneno matano aondolewe alama 2 yaan 2M INSHA
MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA
MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA 1. Mtahiniwa azingatie yafuatayo; Mbinu za kupambana na ufisadi -Kuelimisha wananchi kuhusu madhara ya ufisadi kupitia kwa redio, magazeti, runinga n.k. -Kuwaadhibu wahusika – wapelekwe mahakamani na wafungwa jela. -Wananchi waadilike (wawe na maadili mema). -Viongozi wawajibike katika kazi zao. -Sheria za kupambana na ufisadi zibuniwe na kutekelezwa. -Kubuni nafasi zaidi za kazi -Kuimarisha elimu -Kuongeza mishahara kwa wafanyikazi -Tume zaidi za kukabiliana na ufisadi zibuniwe. SURA YA MAHOJIANO -Insha iwe na kichwa kinacholenga mada -Kuwe na mhoji na mhojiwa -Njia ya maswali na majibu -Njia ya kitamthilia ufuatiwe kwa mfano; Juma: Bakari: TAHADHARI -Atakayefululiza bila kufuata mtindo wa mahojiano aondolewe alama (4) sura baada ya kutuzwa. 2. i) Kilimo cha mboga ii) Upanzi wa miti iii) Utengenezaji wa matofali na kuyauza. iv) Ukarabati wa barabara v) Kushirikiana na polisi katika kutoa usalama kwa umma. 3. Maana ya methali Ikiwa umekwisha jitayarisha kufanya jambo, basi bora ulikabili / ulifanye na ulimalize. -Mtahiniwa aandike kisa kitakachothibitisha ukweli wa methali. -Aonyeshe mtu aliyeanza jambo licha ya vikwazo / matatizo, alijibidiisha kulikamilisha. 4. Sharti mtahiniwa aanze insha kwa maneno aliyopewa bila kubadilisha wala kuongeza. Insha ionyeshe harakati za kumtafuta baba mzazi Asimulie jinsi alivyotambua / alivyokutana na babake kwa mara ya kwanza. Hisia alizozipata kv. Furaha / chuki Iwapo mkutano huu ulifaulisha maisha yake ya usoni au la. Ugunduzi wake ulivyoathiri maisha yake TAZ: Kisa kisimuliwe kwa njia ya kuvutia na kusisimua. Insha
Mwongozo huu unatumika sambamba na mwongozo wa kudumu wa Insha [102/1]
1. Andika hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kupambana na Ufisadi nchini kwa washika dau wote katika Kaunti ya Kakamega. -Insha ihusishe hoja zisizopungua sita kati ya hizi na nyingine zinazorejelea maswala yoyote ya ufisadi nchini: --Chanzo cha ufisadi k.m. umaskini, tamaa, kuiga wengine, kutaka kuhepa adhabu, n.k. --Kunakotokea ufisadi, k.m. ofisini, hospitali, shuleni, mahakamani, katika vyombo vya usafiri, n.k. --Athari za ufisadi k.m. ufujaji wa pesa, nchi/mashirika kutoendelea, n.k. --Adhabu kwa ufisadi k.m. kushikwa, kufungwa, kufutwa, kulazimishwa kulipia, n.k. --Hatua zinazochukuliwa na shirika lake kupambana na ufisadi. --Mapendekezo yake kwa umma kuhusu jinsi ya kupambana na ufisadi. SURA Ionyeshe kuwa ni hotuba kutokana na kianzio, kinachotambua au kuiamkua haadhira. Pia kiishio. Insha yenyewe iandikwe kwa mtiririko ikitumia nafsi ya kwanza. Adhabu ya kawaida ichukuliwe kwa insha isiyochukua sura inayostahili (-04s) 2. Eleza chanzo cha ongezeko la bei ya bidhaa nchini mwako, huku ukionyesha athari za ongezeko hili. CHANZO --Ufisadi --Tamaa --Shilingi ya Kenya kukosa nguvu dhidi ya Dola ya Marekani.
ATHARI
3. Aiszfuye mvua imemnyea. Ni methali. Insha iwe na kisa (au visa) kinachoonyesha ukweli wa methali. Methali ina maana kuwa anayelizungumzia jambo, kulieleza au kulisifu ana tajriba nab. Insha ionyeshe sifa itolewayo na pia alivyonyewa. 4. “Karne ya 21 imeleta ongezeko kubwa la vyombo tofauti vya habari nchini, pamoja na athari anuwai” Jadili kauli hii. ONGEZEKO Insha ithihirishe ukweli kwamba vyombo vya habari vimeongezeka kwa kutoa mifano ya magazeti, majarida, stesheni za redio, runinga, n.k. atakayejaribu kuipinga kauli hii atakuwa amepotoka. ATHARI Ni nzuri na mbaya • Habari zinapatikana kwa urahisi. • Hakuna usiri usiofaa wa serikali tena. • Kuna burudani tele. • Vinaelimisha. • Watu (hususan wale mashuhuri) wamekoseshwa siri katika maisha yao. • Vyombo vingine vinachochea makabila, n.k. • Kuna ongezeko la picha/habari za ngono. • Maadili yamezorota. • N.K. Insha ihusishe hoja zozote sita au zaidi katiya hizi na nyingine. ZIADA YA JUMLA Tumia mwongozo wa kudumu wa insha ili kutuza insha katika viwango kati ya A+ na D-. hoja katika maswali 1,3 na 4 itambulike kwa mkwaju (‘f) kushoto, pembezoni mwa aya iliyobeba hoja. |
Primary Resources
College Resources
|
Secondary Resources
|
Contact Us
Manyam Franchise
P.O Box 1189 - 40200 Kisii Tel: 0728 450 424 Tel: 0738 619 279 E-mail - sales@manyamfranchise.com |