Maswali na Majibu KCSE Kiswahili
Ufahamu | Ufupisho | Isimu Jamii | Insha | Utumizi wa Lugha
UFUPISHO (Alama 15)Vipindi mbalimbali vya historia vimeshuhudia kuibuka kwa magonjwa ya ajabu. Magonjwa hayo yamewahangaisha watu na kuzishughulisha bongo za wanasayansi na madaktari katika kutafuta tiba. Magonjwa kama vile tauni, kifua kikuu, homa ya matumbo na ndui ni baadhi ya yale yaliyotisha sana nyakati fulani za historia ya binadamu. Magonjwa haya yaliwauwa maelfu ya watu na kuibua mifumo na taratibu za maisha ya watu. Hata hivyo , magonjwa hayo yaliweza kuchunguzwa na kutafutiwa tiba kabla ya kumaliza kabisa kizazi cha binadamu. Lakini hii ni baada ya kuwasukuma maelfu ya watu kaburini. Ulimwengu wa sasa unashuhudia janga jingine la maradhi sugu ya ukimwi. Neno ‘UKIMWI’ lilitolewa kutokana na athari za ugonjwa huo mwilini. Neno “UKIMWI” humaanisha ukosefu wa kinga mwilini, ambapo herufi za kwanza za maneno matatu ziliunganishwa pamoja na kuunda neno hilo. Ugonjwa huu ambao tayari umewaua mamilioni ya watu kote ulimwenguni unazidi kuenea kwa kasi, mfano wa moto katika kicheka. Kutokana na kasi yake ya kuua watu, ugonjwa wa UKIMWI umepewa majina kama vile “umeme” na pia “ugonjwa wa vijana”. Watu wengi wanaoambukizwa virusi vya UKIMWI ni wale walio na miaka kati ya 15 hadi 49. Kundi hili kwa kweli ndilo linalohesabiwa kuwa na nguvu za kutunza jamii kwa njia nyingi. Iwapo wengi katika kundi hili watakumbwa na maradhi haya, watasalia wakongwe na watoto wachanga wasioweza kujimudu. Nchini Kenya, UKIMWI uligunduliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka wa 1984. Kufikia mwezi wa Juni 1996, inakisiwa kuwa ugonjwa huu ulikuwa umewaua watu wapatao 65,647 nchini. Hivi sasa, inasemekana kuwa takribani watu zaidi ya 500 hufa kila siku nchini Kenya kutokana na janga hili. Aidha, imedhibitishwa kwamba takriban watu milioni mbili unusu tayari watapoteza maisha yao kutokana na kuaambukizwa virusi vya ugonjwa huu humu nchini. Maradhi haya sasa yamekuwa janga la kitaifa. Kutokana na kuongezeka kwa visa vya UKIMWI, hospitali na zahanati nyingi kote nchini zinashindwa kukidhi mahitaji ya wagonjwa. Kwa hivyo, makundi ya kujitolea na mashirika mbalimbali yameundwa ili kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI. Baadhi ya makundi hayo hutoa tiba ya kisaikolojia pamoja na kuwapa ushauri wa hima ya kuishi, badala ya kukata tamaa. Wagonjwa wengi pia huishia kutibiwa nyumbani kwao. Ugonjwa huu umeathiri jamii kwa njia nyingi. Hali ya maisha na woga, ukosefu wa matumaini, ongezeko la mayatima na kuzorota kwa uchumi kutokana na kutoweka kwa kizazi chenye nguvu za kutoa huduma kwa jamii, na baadhi ya athari za maradhi haya. Lakini jambo la kuzingatia ni hili, tujifunze kutokana na historia.Tuwe na matumaini kwamba siku moja, tiba ya ugonjwa huu itapatikana. Hii ni kwa sababu tumethibitishiwa haya kutoka katika historia yetu wenyewe. Ikiwa magonjwa yaliyosababisha vifo vya wengi kutokana na ukosefu wa tiba yalitokomezwa kupitia juhudi za kimatibabu, sembuse huu ugonjwa tulio nao sasa? Huku tukijikinga kutokana na maradhi haya, tusife moyo bali tuwe na matumaini kwani subira hufuta heri. a) Kwa kutumia maneno yako mwenyewe na bila kupoteza maana, fupisha aya nne za mwanzo (maneno 90 - 100) (alama 3 kwa mtiririko) (alama 12 ) Nakala chafu/maadalizi ……………………………………… Jibu ……………………………………………………………… b) Eleza mambo yanayoleta matumaini kwa wagonjwa wa ukimwi kulingana na aya tatu za mwisho (maneno 40- 45) (alama 1 kwa mtiririko) Nakala chafu …………………………………………………… Nakala Safi ………………………………………………………………… MWONGOZO
UFUPISHO a) i) Vipindi mbalimbali vya historia vimeshuhudia kuibuka kwa magonjwa ya ajabu- tauni, kifua kikuu, homa ya matumbo n.k. ii) Magonjwa haya yamewahangaisha watu na kuzishughulisha bongo za wanasayansi na madaktari katika kutafuta tiba. iii) Magonjwa haya yaliwaua maelfu ya watu na kutibua mifumo na taratibu za maisha ya watu / yaliwaua watu wengi. iv) Magonjwa hayo yaliweza kuchunguzwa na kutafutiwa tiba. v) Ulimwengu wa sasa unashuhudia janga jingine la maradhi sugu ya ukimwi. vi) Ukimwi unazidi kuenea kwa kasi. Umewaua mamilioni ya watu kote ulimwenguni. vii) Ukimwi unazidi kuenea kwa kasi ulimwengu (lazima wazo la kazi litokee). viii) Wengi wa walioambukizwa ni kati ya miaka 15 – 49 ix) Kundi hili lina nguvu / linatunza jamii / wanaosalia ni watoto na wakongwe wanaoachwa. x) Ukimwi uligunduliwa Kenya mwaka wa 1984 (lazima ataje Kenya). xi) Watu zaidi ya 500 hufa kila siku xii) Ukimwi sasa ni janga la kitaifa. b i) Mashirika na makundi ya kujitolea kuwahudumia wagonjwa ii) Makundi hutoa tiba ya kisaikolojia na kuwapa ushauri na hima ya kuishi badala ya kukata tamaa. iii) Wengi hutibiwa nyumbani kwao. iv) Matumaini ya tiba kutokea.
0 Comments
Ukiwa mtoto unadhani ulimwengu ni kipande kimoja cha keki kilicho kitamu mithili ya asali.17/12/2023 Jibu makala yafuatayo kisha ujibu maswali.UFUPISHO Ukiwa mtoto unadhani ulimwengu ni kipande kimoja cha keki kilicho kitamu mithili ya asali. Hakuna dhiki, hakuna mateso, hakuna kuhuzunika kwa ama yoyote. Neno huzurn linasikika masikioni kama neno lisiloelekea kwenye uhalisia wowote. Kwa watoto duma imejaa raha, starehe na vcheko visivyoisha. Maisha ni ahadi njema, yenye matokeo ya kufurahisha na kustarehesha tu sio kudhikisha na kuhuzunisha. Huyu tunayemzungumzia hapa ni mtoto mdogo ambaye hajajua kubainisha kitendekacho mkono wake wa kushoto wala idle kinachofanyika hasa katika mkono wake wa kulia. Hata hivyo, jinsi mtoto anavyoendelea kukua na kufahamikiwa na mambo, vigambo na kadhia zinazoendelea katika mazingira yake, anabainikiwa na mengi machungu ambayo huleta huzuni, sb raha. Hebu tuanze na nyumbani kwao mtoto. Aghalabu, watoto wote hupendwa kwao nyumbani, iwapo wazazi wao ni watu wangwana na wana nafasi ya kulea watoto wao bila taabu. Hata hivyo watoto huchapwa pale wanapokuwa watundu, jambo ambalo huwahuzunisha sana, japo ni wajibu wa wazazi sababu, kama isemwavyo, meha mwana kulia hulia yeye. Pili, inajulikana wazi kwamba watoto wengi siku hizi huenda shule. Huko shule, wao hupendelea sana kucheza kuliko kusoma. Iii wasome kama inavyotakikana, m sharti waelekezwe barabara katika njia hiyo na walimu wao. Katika kuelekezwa huku, walimu wanaweza kulazimika kuwaacthibu, hasa wale watoto ambao huzembea na kutofanya kazi zao wanazopewa kufanya nyumbani kama kawaida ya mfumo wa shule ulivyo. Watoto wa ama hii wanapotiwa adabu raha hujitenga na buzuni huwatawala. Huzuni, hivyo basi, maonekana ya kuwa m uso wa pili katika maisha ya wanadamu, uso wa kwanza ukiwa raha. Na kwa hakika wanaohuzunika si watoto peke yao. Kila mtu duniani ni sharti, katika wakati mmoja au mwingine, azongwe na huzuni. Inajulikana wazi kwamba wanadamu wote hawapendi huzuni asilani na hakika kabisa, kila binadamu huchukia huzuni na kustahabu raha. Hata hivyo, raha humjia binadamu kwa nadra sana, ilhali huzuni humvamia wakati wowote, hata akiwa yumo katikati ya kustarehe. Si tu, inajulikana dhahiri kwamba hakuna mtu asiyewahi kuonja huzuni, japo wapo wengi kweli kweli wasiowahi kuonja raha maishani mwao. Zingatia mtoto anayezaliwa, halafu wazazi wake wanaaga dunia, pengine katika ajali, kabla mtoto mwenyewe hajaweza kujikimu. Mtoto huyu anaishi kutegemea jamaa za wazazi wake. Watu hawa wasipokuwa na nafasi wao wenyewe kimaisha pamoja na ukarimu unaohitajika basi mtoto anateseka na kuhuzunika sana katika maisha yake yote. Ama zingatia mtoto anayetupwa na mamake kijana, anayempata bila kupanga. Hata mtoto huyu akiokotwa na kulelewa na wahisani, maisha yake yatakuwa ya taabu, dhiki na huzuni. Au zingatia mtoto anayelelewa na mama wa kambo anayeondokea kuwa mwovu. Mtoto huyu atakayoijua ni huzuni tu. Ama zingatia mtoto ambaye babake ni mievi na analojua ni kurudi nyumbani usiku akiimba nyimbo za kilevi, kuita mkewe kwa sauti kubwa, kuitisha chakula na kufurahia kupiga watoto wote na mama yao ndipo apate usingizi mnono. Mtoto mwenye baba wa ama hiyo atakayoijua ni huzuni tu, si raha asilani. MASWALI (a) Ukitumia maneno yako mwenyewe na bila kupoteza maana, fupisha aya nne za mwanzo. (Maneno-100). (Alama 9) Nakala chafu ………………………………………………………………………………………………… Nakala safi ………………………………………………………………………………………………… (b) Ukizingatia aya ya mwisho eleza hali mbalimbali zinazowatia watoto buzuni. (Maneno 40-45) (Alama 4) Nakala chafu ………………………………………………………………………………………………… Nakala safi ………………………………………………………………………………………………… Majibu
Majibu (a) (i) Mtoto hudhani/hufikiri ulimwengu umejaa raha na hauna huzuni/hauna mateso/haudhikishi. (ii) Mtoto huyu ni yule mdogo ambaye hajajua kubainisha mambo. (iii) Anavyoendelea kukua, anafahamishwaanabainikiwa na mengi yaletayo huzuni. (iv) Nyumbani ingawa hupendwa, huadhibiwa wanapokuwa watundu na kuhuzunika. (v) Shuleni wanapozembea kazi, wanaadhibiwa na hili huwahuzunisha. (vi) Huzuni basi ni uso wa pili katika maisha ya binadamu, uso wa kwanza ukiwa raha. (vii) Kila mtu duniani huzongwa na huzuni / huhuzunika (viii) Raha humjia mwanadamu kwa nadra ilhali huzuni humuvamia wakati wowote. (ix) Wako watu wengi wasiowahi kuonja raha maishani mwao (Hoja 9-al-1 =9) (b) (i) Mtoto anapofiwa na wazazi (ii) Mtoto anayetupwa na mamake kijana baada ya kuzaliwa. (iii) Mtoto anayelelewa na mama wa kambo mwovu. (iv) Mtoto ambaye babake ni mlevi Hoja4-Al-1 —4 Soma makala haya kisha ujibu maswali yafuatayo HAKI ZA BINADAMU Binadamu wana mazoea ya kufikiria kuwa jinsi wafanyavyo, waongeavyo na wafikiriavyo kuhusu vitu ndivyo inavyopasa kuwa. Kama binandamu tunaamini njia yetu ndiyo sahihi, yenye mantiki na inayopasa kufuatwa na kila mtu. Msingi huu huu unakwenda kinyume na kutambua kila binadamu ana haki ya kufikiri, kusema au kuongea na kutenda mradi asikiuke haki ya mwenzake iliyo sawa na yake. Nguzo mojawapo inayogongomelea hoja hii ni Haki za Binadamu. Azimio kutangaza Haki Bia za Binadamu liliafikiwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Desemba 1948. Baraza kuu hilo liliyasisitizia mataifa wanachama umuhimu wa kuyasambaza, kuenezea, na kusisitiza kusambazwa kwa azimio hilo katika shule na taasisi za kielimu. Msingi wa uhuru, haki na amani ulimwenguni ni kutambua binadamu wote wana haki sawa. Ingawa kimsingi jamii na mataifa yote ya ulimwengu yanapaswa kuthamini, kusambaza na kuhimiza umuhimu wa Haki za Binadamu zipo jamii ambazo hukiuka haki hizo. Matokeo ya ukiukaji huu yana athari hasi sana kama ilivyotokea nchini Rwanda na Bosnia. Herzegovina kulikotokea mauaji ya halaiki. Azimio la Haki za Binadamu linajumuisha vipengele kadha ambavyo ni mihimili mikuu ya Azimio lenyewe. Kipengele msingi kabisa kinasisitiza kuwa kila kiumbe anazaliwa huru na ana haki na hadhi sawa na kiumbe mwingine. Ukweli wa kauli hii ulikokotezwa na kauli ya mwanafalsafa maarufu Jean Jacques Rosseau aliyesema kuwa kila kiumbe huzaliwa huru lakini huwa katika pingu ulimwengu mzima. Kauli hii ilitambua ukiukaji huu wa kipengele hiki. Kipengele cha pili kinasisitiza kuwa binadamu wote wana haki za kufurahia uhuru wao pasi na kutengwa au kubezwa kwa misingi yoyote ile si rangi, kabila, jinsia, lugha, dini, asilia, utajiri au chochote kile. Vipengele vingine vinatukumbusha kuwa kila mtu ana haki ya kuishi na kupata ulinzi. Hamna mtu anayepaswa kuishi maisha ya utumwa au unyonge wa kutumikishwa kwa namna yoyote ile. Suala hili linasisitizwa na kipengele cha sita kinachokataza kudhalilishwa kwa watu au kutunzwa kwa namna yoyote ambayo inamfedhehesha kama kiumbe. Azimio la Haki za Binadamu linasisitiza kuwa binadamu yoyote nyule ana haki ya kupata ulinzi wa kisheria. Binadamu huyo hapaswi kubaguliwa na ana haki ya kupata fidia ya kisheria taraa haki zake za kimsingi zikikiukwa. Hata hivyo sio watu wote ulimwenguni ambao wanazifurahia haki hizi za kimsingi. Zipo lukuki za jamii ulimwenguni ambako haki za kimsingi zinakiukwa. Katika nchi ambazo zinaongozwa na watawala wa kiimla, si ajabu kuona haki za binadamu zikikiukwa. Viongozi wa aina hiyo huwa wamegeuzwa ng’ombe wa shemere na tamaa, ubinafsi na ukatili usiojua thamani ya utu. Viongozi wa aina hii wanasahau kuwa kila binadamu ana haki ya kuishi maisha huru, asipotumikishwa wala kulanguliwa kama bidhaa. Nchi za kiimla aghalabu huongozwa na itikadi kuwa kiongozi ndiye pekee ambaye ana uwezo wa kufikiri, kuamua na kutenda. Watu wengine wanapaswa kumfuata kisilka kama yule mbwa wa Pavlov ambaye alitokwa na mate kila kengele ilipopigwa. Viongozi wa ama hii hawachelei kuwatenza nguvu raia zao: Kuwadhalilisha kwa namna nyingi. Viongozi wa aina hiyo huiona sheria ya nchi kama iliyowekwa kwa watu wengine bali sio wao. Msimamo huu unakwenda kinyume na kipengele cha saba cha Haki Bia za Binadamu kisemacho kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria. Baadhi ya haki zinazokiukwa katika jamii za kimabavu ni haki ya watu kuungana, kuwaza, kushiriki katika maamuzi ya serikali, kuwa mwanachama wa jumuia waitakayo, kumiliki mali, kutembea, kuishi anakotaka kutohukumiwa bila ya kuwako na utaratibu wa kisheria. Ni muhimu hata hivyo kujua ni muhimu kwa raia wenyewe kujielimisha na kuzijua haki zao. Serikali inapaswa kuwa mlinzi wa sheria zenyewe. Lakini muhimu kujua pia kuwa mlinzi naye hulindwa pia. Maswalia) Kwa maneno kati ya 90 – 100 fafanua Haki Bia za Binadamu zilizoafikiwa na Baraza kuu la umoja wa Mataifa. (alama 10) Nakala Chafu __________________________________________________________________________ Nakala Safi __________________________________________________________________________ b) Kwa nini viongozi wa kiimla hukiuka haki za binadamu. (Maneno 50 – 60). Nakala Chafu __________________________________________________________________________ Nakala Safi __________________________________________________________________________ Mwongozo
a) Kwa maneno kati ya 90- 100 fafanua Haki Bia za Binadamu Zilizoafikiwa na Baraza kuu la Umoja wa mataifa Kila kiumbe anazaliwa humu na ana haki na hadhi sawa na kiumbe mwingine’ • Binadamu wote wana haki za kufurahia uhuru wao pasi na kutengwa au kubezwa kwa misingi yoyote ile si rangi, kabila, jinsia, lugha, dini, asilia au chochote kile. • Kila mtu ana haki ya kuishi na kupata ulinzi • Hamna mtu anayepaswa kuishi maisha ya utumwa, kutumikishwa, kudhalilishwa au kutunzwa kwa namna inayomfedhehesha kama kiumbe. • Haki ya kupata ulinzi wa kisheria • Kutobaguliwa na ana haki ya kupata fidia ya kisheria taraa haki zake za kimsingi zikikiukwa . Alama 8 utiririko alama 2) b) Kwa nini viongozi wa kiimla hukiuka haki za binadamu • Tamaa ya uongozi • Ubinafsi • Ukatili, hawajui thamani ya utu • Kiburi cha kujiona kuwa wao ndio wanaofahamu mambo zaidi • Husahau kuwa binadamu ana haki ya kuishi maisha huru bila kutumikishwa au kutanguliwa kama bidhaa • Hudhani wao tu ndio wana uwezo wa kufikiri, kuamua na kutenda na wananchi wanapaswa kufuata tu • Huona kuwa sheria ya nchi imewekewa wengine na wala sio wao hivyo huwatenza nguvu raia zao Alama 4, utiririko alama 1) UFUPISHOVipindi mbalimbali vya historia vimeshuhudia kuibuka kwa magonjwa ya ajabu. Magonjwa hayo yamewahangaisha watu na kuzishughulisha bongo za wanasayansi na madaktari katika kutafuta tiba. Magonjwa kama vile tauni, kifua kikuu, homa ya matumbo na ndui ni baadhi ya yale yaliyotisha sana nyakati fulani za historia ya binadamu. Magonjwa haya yaliwauwa maelfu ya watu na kuibua mifumo na taratibu za maisha ya watu. Hata hivyo , magonjwa hayo yaliweza kuchunguzwa na kutafutiwa tiba kabla ya kumaliza kabisa kizazi cha binadamu. Lakini hii ni baada ya kuwasukuma maelfu ya watu kaburini. Ulimwengu wa sasa unashuhudia janga jingine la maradhi sugu ya ukimwi. Neno ‘UKIMWI’ lilitolewa kutokana na athari za ugonjwa huo mwilini. Neno “UKIMWI” humaanisha ukosefu wa kinga mwilini, ambapo herufi za kwanza za maneno matatu ziliunganishwa pamoja na kuunda neno hilo. Ugonjwa huu ambao tayari umewaua mamilioni ya watu kote ulimwenguni unazidi kuenea kwa kasi, mfano wa moto katika kicheka. Kutokana na kasi yake ya kuua watu, ugonjwa wa UKIMWI umepewa majina kama vile “umeme” na pia “ugonjwa wa vijana”. Watu wengi wanaoambukizwa virusi vya UKIMWI ni wale walio na miaka kati ya 15 hadi 49. Kundi hili kwa kweli ndilo linalohesabiwa kuwa na nguvu za kutunza jamii kwa njia nyingi. Iwapo wengi katika kundi hili watakumbwa na maradhi haya, watasalia wakongwe na watoto wachanga wasioweza kujimudu. Nchini Kenya, UKIMWI uligunduliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka wa 1984. Kufikia mwezi wa Juni 1996, inakisiwa kuwa ugonjwa huu ulikuwa umewaua watu wapatao 65,647 nchini. Hivi sasa, inasemekana kuwa takribani watu zaidi ya 500 hufa kila siku nchini Kenya kutokana na janga hili. Aidha, imedhibitishwa kwamba takriban watu milioni mbili unusu tayari watapoteza maisha yao kutokana na kuaambukizwa virusi vya ugonjwa huu humu nchini. Maradhi haya sasa yamekuwa janga la kitaifa. Kutokana na kuongezeka kwa visa vya UKIMWI, hospitali na zahanati nyingi kote nchini zinashindwa kukidhi mahitaji ya wagonjwa. Kwa hivyo, makundi ya kujitolea na mashirika mbalimbali yameundwa ili kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI. Baadhi ya makundi hayo hutoa tiba ya kisaikolojia pamoja na kuwapa ushauri wa hima ya kuishi, badala ya kukata tamaa. Wagonjwa wengi pia huishia kutibiwa nyumbani kwao. Ugonjwa huu umeathiri jamii kwa njia nyingi. Hali ya maisha na woga, ukosefu wa matumaini, ongezeko la mayatima na kuzorota kwa uchumi kutokana na kutoweka kwa kizazi chenye nguvu za kutoa huduma kwa jamii, na baadhi ya athari za maradhi haya. Lakini jambo la kuzingatia ni hili, tujifunze kutokana na historia.Tuwe na matumaini kwamba siku moja, tiba ya ugonjwa huu itapatikana. Hii ni kwa sababu tumethibitishiwa haya kutoka katika historia yetu wenyewe. Ikiwa magonjwa yaliyosababisha vifo vya wengi kutokana na ukosefu wa tiba yalitokomezwa kupitia juhudi za kimatibabu, sembuse huu ugonjwa tulio nao sasa? Huku tukijikinga kutokana na maradhi haya, tusife moyo bali tuwe na matumaini kwani subira hufuta heri. a) Kwa kutumia maneno yako mwenyewe na bila kupoteza maana, fupisha aya nne za mwanzo (maneno 90 - 100) (alama 3 kwa mtiririko) (alama 12 )
Nakala chafu/maadalizi ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… b) Eleza mambo yanayoleta matumaini kwa wagonjwa wa ukimwi kulingana na aya tatu za mwisho (maneno 40- 45) (alama 1 kwa mtiririko) Nakala chafu ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… Nakala Safi ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… |
Primary Resources
College Resources
|
Secondary Resources
|
Contact Us
Manyam Franchise
P.O Box 1189 - 40200 Kisii Tel: 0728 450 424 Tel: 0738 619 279 E-mail - sales@manyamfranchise.com |