Jadili nafasi ya sehemu zifuatazo katika riwaya ya Chozi la Heri:(a) Hotuba (alama 10)
(a) Hotuba (alama 10)
Hotuba ni maelezo maalumu yanayotolewa na mtu mmoja mbele ya watu. Pia huitwa hutuba. Mwandishi wa riwaya hii ametumia hutuba kwa ustadi mkuu kupitisha ujumbe mbalimbali. Hotuba hizi ni:
1. Hotuba ya Racheal Apondi kwa maafisa waliohudhuria warsha kuhusu jukumu la vikosivya askari katika kudumisha usalama, amani na maridhiano nchini (uk 112- 113). Katika hotuba hii, Racheal Apondi anasisitiza kuwa:
Suala la usalama haliwezi tena kupuuzwa. Usalama umekuwa moja wapoyamahitajiyakibinadamu. Anasema kuwa bila usalama, binadamu hawezi hata kushiriki katika shughuli za kuzalisha mali, hivyo hata mahitaji yake mengine ya kimsingi kama vile chakula, malazi na makazi haya wezi kukidhiwa. Kila binadamu ana jukumu la kudumisha amani na usalama. Wafanyakazi wa umma, hasa polisi na wanajeshi wana jukumu kubwa zaidi la kudumisha usalama na amani. Kila mmoja wetu anastahili kuhakikisha kuwa ameepuka vitendo vya kihalifu. Ni vyema mtu kuwaangaza wahalifu wakati wote. Vikosi vya polisi na wanajeshi vimefunzwa maarifa ya kukabiliana na kadhia za Jinai na upelelezi. (4×1= 4)
2. Hotuba ya Lunga Kiriri- Kangata kwa walimu na wanafunzi gwarideni (uk 68-69). Hotuba hiii lisisitiza umuhimu wa kuhifadhi mazingira. Anasisitiza kuwa:
Suala la uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. Misitu ilikuwa imevamiwa na viongozi wenye mate yafisi. Baadhi ya vinara wa taasisi mbalimbali za umma wamewaacha Wanyama kama mayatima kwa kuwap okama kazi yao. Maelfu ya maekari ya misitu yamefyekwa na kujengwa viwanda. Badala ya mibamba kofi na miti mingine inayosafisha hewa, micha iimetwaa nafasi yake. Wanaohusika na matendo haya wanapoulizwa hudai kuwa michaisia duiya mazingira! Wengine wanasema kuwa misitu haina budi kukatwa ili kupanda mimea inayotoa chakula, kwani jamii lazima ijitosheleze kwa chakula. La kuhuzunisha ni kwamba hawa hawa wanaosema hivyo ndio wanaokita majengo ya kifahari katika sehemu ambazo zinastahili kutengewa upanzi wa chakula! Wengine wamediriki kunyakua hata madhabahu kwenye Mlima wa Nasibu ili kujenga hoteli kubwa za kitalii. Wazee wetu hata hawana mahali pa kuchomea kafara! Tuna kata miti bila kupanda smingine. Hata mabustani ya maua tunashindwa kuyastawisha. Tukiendelea kuharibu mazingira sehemu yetu itazidi kuwa jangwa. (2×1= 2)
3. Hotuba ya Umu katika hoteli ya Majaliwa siku ya key akuzaliwa.
Umu ana washuku Mwangeka na Apondi kwa kuwa wazazi wake wema. Ana washukuru kwa kumsomesha. Anawashukuru kwa kumsaidia Dick kujiendeleza kimasomo. Mwangeka na Apondi wanamshukuru Umu kwa kuwapa furaha. Apondi anamshukuru kwa kumlea mdogo wao kwa maadili bora. (2×1= 2)
4. Hotuba ya Dick katika hoteli ya Majaliwa siku ya kuzaliwakwaUmu.
Dick anamshukuru Umu kwa msaada wake na ahadi ya kumlea. Anamkumbusha siku walipokutana katika uwanja wa ndege na ilivyokuwa muhimu kwake. Anamshukuru Umu kwa kumwelekeza kwa wazazi wao wale. Anawashukuru Apondi, Mwangeka na wanawe kwa ushauri wanaompa. (2×1= 2) Mtahiniwa ataje hotuba kisha aeleze masuala muhimu yanayoibuliwa na kila moja. (b) Uozo katika jamii (alama 10)
(b) Uozo katika jamii (alama 10)
Uozo ni hali ya kuzorota na kutozingatiwa tena kwa maadili mema katika jamii. Ni hali ambapo mila zote na desturi njema huvurugwa na wanajamii wanaofanya mambo yaliyo kinyume na hali hali si yamaisha. Mwandishi amejadili suala hili kwa undani kama ifuatavyo; Jamii inaendeleza ubakaji. Genge la mabarobaro watano lilifululiza hadi walipokuwa maskini Lime naMwanaheri na kuwabaka mbele ya baba yao (uk 25). Kuna ulanguzi wa dawa za kulevya. Dick alipotoroshwana Sauna alipelekwa kwa Tajiri mmoja aliyemwingiza katika kusafirisha dawa za kulevya kutoka nchi moja hadi nyingine (uk 119- 120). Wanajamii wanaendeleza uporaji na wizi wa mali. Vijana wana wavamia watu, kuwaua na kupora katika maduka ya kihindi, kiarabu naya wa afrika wenzao. Jamiii naendeleza ufuska/ ukahaba. Sauna aliiba Watoto na kuwapeleka kwa mama mmoja aliyewatumia kwa biashara yanipe ni kupe (uk 84).
Biashara haramu inaendelezwa. Bi. Kangara alifanya biashara ya kuwa uza Watoto na vijana- Safari yake ilipata mkondo mwingine baada ya polisi kupata fununu kuhusu njama ambazo yeye na Bi. Kangara walikuwa wakiendesha. Mabibi hawa walikuwa na mtandao ambao kazi yake ilikuwa kuwauza Watoto na vijana (uk 84).
Kuna tatizo la mimba za mapema. Vijana wana mazoea ya kukumbatia mtafaruku wa kuhisia unaowapatana mara hujipata wameambulia ujauzito kama alivyofanya Zohali (uk 98). Baadhi ya wanajamii wanaendeleza uavyaji mimba. Sauna alijaribu awezavyo kuavya mimba na mwishowe, baada ya kushindwa, anaamua kujiua. Kukiuka maadili ya kikazi. Fumba (mwalimu) anakiuka maadili ya kazina kujihusisha kwa mapenzi na mwanafunzi wake, Rehema, na hatimaye kumpachika ujauzito (uk 102). Wazazi wana wabaka wana wao. Babake Sauna anafanya mapenzi na mwanawe kila apatapo nafasi, na mwishowe, Sauna anapata mimba. Starehe na anasa kwa vijana. Vijana wa vyuo vikuu wameshindwa kutofautisha usiku na mchana. Tindi anasahau kumrejesha Lemi nyumbani kutokana na muziki (uk 121). Wazazi wanakwepa malezi na kuwatupa wanao wakiwa wachanga. Neema anampeleka mtoto aliyemwokota kwapolisi (uk 162). Vijana kuwaiga wazee. Mwangemi na Mwangeka walikuwa na tabia mbovu yakumuiga babu yao (uk 186).
(10×1= 10)
Mtahiniwa afafanue kwa mifano kutoka katika riwaya
0 Comments
“Nyamaza wewe! Nyinnyi ndio mnaoturudisha nyuma miaka yote hii!”(a) Eleza muktadha wa dondoo (alama 4)(b) Kwa kurejelea hoja saba, eleza jinsi msemaji alivyorudishwa nyuma (alama 7)( c) Eleza umuhimu wa msemaji katika riwaya (alama 6)(d) Eleza toni ya dondoo hili (alama2)(e) Toa sifa moja ya msemaji katika dondoo hili. (alama1)“uuuui! Uuuui! Jamani tusaidieni! Uuuui! Uuuui! Mzee kedi usituue, sisi tu majirani! Maskini wangu!”a)Elezea muktadha w dondoo hili.(Al 4)
a)Elezea muktadha w dondoo hili.(Al 4)
Ni kumbukumbu ya Ridhaa akikumbuka kilio cha mkewe terry Ridhaa akiwa nje ya jumba lake liliochomeka, na hiki ni kilio cha mkewe wakati walipoangamia kwa mkasa wa moto huo. b) Fafanua tamathali ya usemi huu(Al 2)
b) Fafanua tamathali ya usemi huu(Al 2)
tanakali ya sauti – uuuuwi! Uuuuwi! c) taja mambo yaliyofanyikia Ridhaa awali ya kuashiria mikasa. (Al 4)
c) taja mambo yaliyofanyikia Ridhaa awali ya kuashiria mikasa.(Al 4)
b) Kwa kurejelea riwaya ya chozi la heri jadili dhiki za wakimbizi.(Al 10)
Kwa kurejelea riwaya ya chozi la heri jadili dhiki za wakimbizi
Eleza ufaafu wa anwani ya chozi la heri (Al 20)Eleza ufaafu wa anwani ya chozi la heri Chozi ni majimaji yanayotoka kwenye jicho la mtu kutokana na maumivu au furaha. Heri ni hali ya kuwa salama au nafuu au afadhali. Kwa hivyo, chozi la heri ni chozi la nafuu. Maana ya kijanda/kiistari ni maisha ya mhusika kubadilika kutoka hali mbaya hadi hali nzuri. Kwa mfano:
“Vipi, binadamu anavyoweza kuyazoa maji yaliyomwagika?”a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
b) Tambua mbinu ya lugha iliyotumika (alama 2)
Swali balagha - vipi, binadamu anavyoweza kuyazoa maji yaliyomwagika ? alama 2
c) Jadili sifa tatu za msemaji. (alama 3)
d) Hakiki jinsi binadamu alivyomwagikiwa na maji katika riwaya (alama 11)
Mwandishi amejadili kwa kina maudhui ya mapuuza. Thibitisha . (alama 20)Mwandishi amejadili kwa kina maudhui ya mapuuza. Thibitisha . (alama 20)
MAISHA YANGU YALIJAA SHUBIRI TANGU UTOTONI.I. ELEZA MUKTADHA WA MANENO HAYA. (ALAMA 4)
II. FAFANUA MBINU MBILI ZA LUGHA ZILIZOTUMIKA KATIKA DONDOO HILI. (ALAMA 4)
iii. Jadili jinsi mwandishi amesawiri suala la ukatili. (alama 12)
Riwaya ya Chozi la Heri imejaa aina mbalimbali za migogoro. Jadili. (alama 10)Riwaya ya Chozi la Heri imejaa aina mbalimbali za migogoro. Jadili. (alama 10)
Jadili dhana ya Chozi katika riwaya ya Chozi laHeri. (alama 10)a) Jadili dhana ya Chozi katika riwaya ya Chozi laHeri. (alama 10)
‘TAWALA WAHAFIDHINA TAWALA, MWANZI WETU TAWALA…. ‘A) ELEZA MUKTADHA WA DONDOO HILI . (ALAMA 4)
a) Eleza muktadha wa dondoo hili . (alama 4)
B) NI MBINU GANI IMETUMIKA HAPA. (ALAMA 2)
b) Ni mbinu gani imetumika hapa. (alama 2)
c) Eleza makosa saba ya maneno haya. (alama 14)
Ukabila ni tatizo sugu katika nchi nyingi za Kiafrika. Tetea kauli hii ukilejelea Chozi la Heri ( al. 20)
“ Kwa kweli ni hali ngumu hii”
mwongozo
Weka dondoo katika muktadha wake. (al.4)
Ni hali gani inayorejelewa kwenye dondoo. (al.6)
Nimeondoka. Acha nitambe na ulimwengu, huenda nikaambulia cha kukusaidia kuikimu familia. Nasikitika kwa uchungu nitakaokusababishia wewe na wanaoa) Eleza muktadha wa maneno haya. (alama 4)
b) Kwa kutolea mifano miwili, taja tamathali ya lugha iliyotumika. (alama 3)
Nahau
c) Jadili machungu yaliyompata binti yake msemaji. (alama 7)
d) Eleza umuhimu wa kituo cha Benefactor. (alama 6)
“Baba, umewahi kumwona mtoto wa miaka hamsini ambaye hajasota…………”a) Eleza muktadha wa dondo hili. (alama 4)
(i) Msemaji – Tila
(ii) Msemewa – Ridhaa (anapowaza baada ya nyumba kuchomeka). (iii) Mahali – mawazoni Ridhaa (iv) Ridhaa anapotazamana na majivu ya familia yake ndipo anakumbuka mazungumzo kati yake na mwanawe Tila (Hoja 4 x 2 = 8) b) Taja mbinu iliyotumika (alama 2)
Jazanda – mtoto wa miaka hamsini ambaye hajasota kumaanisha kukwama kimaendeleo (mafanikio baada ya uhuru) ( 1 x 2 = 2)
c) Fafanua sifa za mzungumzaji. (alama 4)
Sifa za Tila
i) Ni msomi – anaelewa maswala ya sheria kwa kina ii) Ni mzalendo – anasema wanahitaji kiongozi ambaye atapeleka jahazi kwenye visiwa vya hazina. iii) Amepevuka – anajua nguvu za vijana ni kama nanga. iv) Amezinduka – anajua kwamba bado wahafidhina hawajapata uhuru. Zozote 4 x 1 = 4 d) Jamii ya msemewa imekumbwa migogoro chungu nzima. Thibitisha. (alama 10)
Anwani “Chozi la Heri” ni kinaya .Thibitisha (alama 10)a) Anwani “Chozi la Heri” ni kinaya .Thibitisha (alama 10)
b) dondoamaudhuikutoka kwa wimbo wake Shamsi.
“La muhimu ni mtu kujifocus tu. Mimi najua japo …..baada ya kupona magonjwa nitaendelea na masomo yangu.”a) Liweke dondoo hili katika muktadha wake. (alama 4) b) Tambua maudhui mawili yanayojitokeza katika dondoo hili huku ukiyatolea mifano. (alama 4) c) Jina la msemaji ni la kimajazi, eleza. (alama 2) d) Umihimu wa msemaji. (alama 6) e) Tambua tamathali za usemi zinazotokana na dondoo hili. (alama 4) mwongozo“La muhimunimtukujifocustu. Mimi najuajapo …..baada ya kuponamagonjwanitaendelea na masomo yangu.”
a) Liwekedondoohilikatikamuktadha wake. (alama 4) Maneno yalisemwa na Tuama, akimwambiaSelume na Meko ,kwenyekituo cha mwanzompya, akijaribukuwaambiakuwakupashwatoharasisiomwisho wa masomo. b) Tambuamaudhuimawiliyanayojitokezakatikadondoohlihukuukiyatoleamifano. (alama 4) c) Jina la msemaji ni la kimajazi, eleza (alama 2) Tuama- kusaliamahalipamojabilakusonga.,anashikiliamila na desturizilizopitwa na wakatikamatohara. d) Umihimuwamsemaji. (alama 6) e) Tambuatamathalizausemizinazotokananadondoohili. (alama 4) Kuchanganyandimi-ni mtukujifocustu Taharuki- hatujuikamaTuamaaliendelea na masomo. |
Uchambuzi wa Chozi la Heri na Assumpta K MateiCATEGORY
ARCHIVES
AUTHOR
M.A NYAMOTIB.ed Science [MKU] RSS FEEDS
CHOZI LA HERI![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
|