Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswaliKama dau baharini, duniya inavyoyumba, Limeshamiri tufani, kila mmoja lakumba, Viumbe tu hali gani! Duniya yatishika, utahisi kama kwamba, Vilima vyaporomoka, na kuvurugika myamba, Viumbe tu hali gani! Tufani hilo la kusi, languruma na kutamba, Linapuliza kwa kasi, hapana kisichoyumba, Viumbe tu hali gani! Mujiwe ni kubwa sana, mfanowe kama nyumba, Yazuka na kugongana, wala hatuna la kwamba, Viumbe tu hali gani! Mibuyu hata mivule, kama usufi na pamba, Inarusha vilevile, seuze hiyi migomba Viumbe tu hali gani! Ni kipi kilotuliya, tuwazeni na kudumba, Mandovu kiangaliya, yagongana na masimba, Fisi wako hali gani! Hata papa baharini, tufani limewakumba, Walioko mikondoni, kila mmoja asamba, Dagaa wa hali gani! Mashehe wa mdaduwa, kwa ubani na uvumba, Tufani hilo kwa kuwa, kusoze kwake kutamba, Itokee afueni! (Shairi la ‘Tufani’ la Haji Gora Haji, katika Tamthilia ya Maisha, uk 62) Maswali;
0 Comments
|
AuthorAtika School Team Archives
December 2023
Categories
All
|
Can't find what you are looking for? Don't worry, Use the Search Box Below.
Primary Resources
College Resources
|
Secondary Resources
|
Contact Us
Manyam Franchise
P.O Box 1189 - 40200 Kisii Tel: 0728 450 424 Tel: 0738 619 279 E-mail - sales@manyamfranchise.com |