​​Soma shairi hili kisha ujibu maswali
Naingia ukumbuni,nyote kuwakariria
Ushairi niwapeni, hoja nitawaachia Mnipe masikioni, shike nachoelezea, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Naaanza kwa usalendo, nchi yetu tuipende, Yadhihirishe matendo, nchi yetu tuilinde, Wa kila mtu muwendo, usije kawa mpinde, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Wote tuwe na umoja, tuuache ukabila, Kabila lisiwe hoja, mwenza kunyima hela, Taifa letu ni moja, Mkenya ndilo kabla, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Linda demokrasia, uongozi tushiriki, Haki kujielezea, wachotaka na hutaki, Change naweza tetea, demokrasia haki, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili Tena adili usawa, mgao rasilimali, Bajeti inapogawa, isawazishe ratili, Idara zilizoundwa, faidi kila mahali, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Tuwe na uadilifu, twache tamaa ya hongo, Tusiwe na uadilifu, wa kuwa watu waongo, Tukomeshe uhalifu, kisha tuache maringo, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Ubinafsi si adili, ila ni kusaidiya, Ukiwa nayo maali, asiyenacho patiya, Kama mtu mswahili, ubinafsi achiya, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Na invyoelezea, katiba ni kielezi, Tutii kwa mazoea, hadi kijacho kizazi, Kwa hayo nitawachia, hiyo ya ziada kazi, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. MASWALI
MAJIBU
Follow AtikaSchool.Org on our Social ChannelsThis gives you an opportunity to get our latest uodates, changes and firsthand information ushairi questions and answers pdfushairi pdf downloadushairi wa kiswahili pdfushairi noteskiswahili questions and answers pdffasihi simulizi questions and answers
0 Comments
Leave a Reply.Don't give up, Keep Searching for more |
AuthorAtika School Team Archives
January 2023
Categories
All
|