Soma shairi lifuatalo kisha uyajibu maswali.
Mungu naomba subira, subira nayo imani
Imani iliyo bora, bora hapa duniani Duniani mwa kombora, kombora nayo hiani Hiani pamwe ukora wenye kuhini. Kuhini kwenye kiburi, kiburi na ufidhulu Ufidhuli wa kudhuri, kudhuri wangu muwili Muwili hata kiclari, kidari kuwa thakili Thakili kisinawiri, kisinawiri misuli. Misuli kuwa hafifu, hafifu kama muwele Muwele wa hitilafu, hitilafu ya nduwele Nduwele kutakilifu, kutakilifu milele Milele kutoniafu, kutoniafu na vishale. Vishale vinitomele, vitomele vikwato Vikwato pia maole, maole kufanya mito Mito ya matozi tele, tele mithili kitoto Kitoto kilo vipele, vipele vyenye fiakuto. Fukuto lanipa neno, neno hili kutamka Kutamka wazi vino, vino subira kutaka Kutaka imani mno, mno n’sipate wahaka Wahaka wa matukano, matukano na mashaka. Mashaka haya ya leo, leo yawe yamepita Yaniepita na vilio, vilia vipishe nyota Nyota njema ing’arao, ing’arao kunikita Kunikita salamani, salamani nikadata. Maswali
a) Kwa nini nafsi neni inaomba subira na amani? (al.2)
b) Shairi hili ni la aina gani kwa kuzingatia (al.4) (i) Mpangilio wa maneno (ii) Mpangilio wa vina. c) Kwa kutolea mifano eleza mbinu mbili za lugha zilizotumika katika shairi. (al.4) d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha nathari. (al. 4) e) Kwa kutolea mifano, eleza jinsi uhuru wa kishairi ulivyotumiwa kutekeleza arudhi. (al.6) Majibu
(a) Ili asiwe na wasiwasi ya kutukanwa na huhiniwa aepuke kufanyiwa mabaya. 1 x 2 =2
(b) (i) Pindu/mkufu/nyoka (al.1) Kwa sababu neno la mwisho katika mshororo wa mwisho wa ubeti linatumiwa kuanzia ubeti unaofuata. (al. 1) (ii) Ukaraguni (al.1) Vina vya kati na vya mwisho vinatofautiana kutoka ubeti mmoja hadi mwingine. (al.1) (c) (i) Tashbihi - Hafifu kama muwele - Tele mithili kitoto.(al.2) (ii) Uradidi/Takriri - Subira’ - Bora, kombora, ukora - Kiburi, kudhuri n.k.(al.2) (d) (i) Misuli kuwa dhaifu sana kama ya mgonjwa. (ii) Hasa mgonjwa mwenye tatizo la (iii) Ambao unasumbua sana daima na (iv) usiopona kwa vishale. (zote4 x 1 = 4) (e) (i) Inkisari - kuleta urari wa mizani k.m kilo — kilicho. (ii) Tabdila - kuleta urari wa vina k.m. kudhuri — kudhuru maole — maozi. - Kuleta urari wa mizani k.m nduwele — ndwele muwili — mwili (iii) Mazida - kuleta urari wa vina pia mizani. - Vinitomele - vinitome. Kutaja na matumizi (al.1) Mfano (al.1) Zote 3 x 2 = 6
0 Comments
Mkatanimkatika, harithihatorithiwa
Sinaninalolishika, walaninalochukuwa Mlimwengukanipoka, hata tone la muruwa! Mrithininiwanangu? Sinango’ombesinambuzi,sinakondesinabuwa Sinahatamakaazi, mupasayokuyajuwa Sinamazurimakuzi, jinsinilivyoachiwa Mrithininiwanangu? Sinakazisinabazi, ilawingiwashakawa Sinachembeyamajazi, mnonikukamuliwa Nakwa’cheniupagazi, mgumukwenuku’tuwa Mrithininiwanangu?
Sinasikuachajina, mkatahatasifiwa
Hatanifanye la mana, mnonikulaumiwa Poleniwanangusana, sinakwenu cha kutowa Mrithininiwanangu? Sinaleosinajana, sinakeshokutwaliwa Sinazizisinashina, walatawikuchipuwa Sinawanangu mi sana, la kwacha nakuraduwa Mrithininiwanangu? Sina utu sinahaki, milayangumeuliwa Nyumayanguilidhiki, nambeleimekaliwa N’nawananamikiki, hadin’tapofukiwa Mrithininiwanangu? Sinai la keshokwenu,wenyewekuiongowa Muwanekwanyingi,mbinumwendepasikupuwa Leo siyo, keshoyenu, kamamutajikamuwa Mrithininiwanangu? (Kina cha maisha A.S.Mohammed) MASWALI
MAJIBU
a) Hali yamzungumzaji. (al 4)
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Hukuja hapa kwa wingi,
Vitimbi vya kila namna, Kunambia nikuruzuku, Kimwana awe mwenzio, Hukumtwaa mwanangu, Kisema mno walavu, Vipi wangeuza ngoma, Mapepo wampigia? Siwe uloandaa, Harusi ya kukata na shoka, Masafu ya magari, yakilalama jua kali, Hadi kanisani kungia, mimbari wa kusimama, Kasema utamuenzi, hadi yenu mauko? Vipi jicho lageukia, mitaani vipaa mwitu? Hukunabia we fidhuli, Mwanangu utamtunza? Taandamana naye daima, Ja chanda na pete? Hukumwonjesha tamu, ya ulaghai huyuno? Midisko wampleka, kizingizia mapenzi, Vipi wamtezea shere, mwangu kumliza?
Lini taacha dhuluma hizino humfanyiazo,
Tuchukua lini majukumu, Ya kumlea na vifaranga? Huachi kulia u waya Wanao kitelekeza Nadhiri zako za nitakipu promise, Zi wapi mwana balaa? Lini tafumbua maozi, uone huyu nduli, Alotwala wengi wapendi, Kwa jicho la nje kuwangia, Imeanguka miamba mingapi, nayo ngangania kufia dodani, Zinduka mwana zinduka, Ailayo waangamiza. Maswali
majibu
Shairi la pili Majibu
Soma shairi hili kisha ujibu maswali
Naingia ukumbuni,nyote kuwakariria
Ushairi niwapeni, hoja nitawaachia Mnipe masikioni, shike nachoelezea, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Naaanza kwa usalendo, nchi yetu tuipende, Yadhihirishe matendo, nchi yetu tuilinde, Wa kila mtu muwendo, usije kawa mpinde, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Wote tuwe na umoja, tuuache ukabila, Kabila lisiwe hoja, mwenza kunyima hela, Taifa letu ni moja, Mkenya ndilo kabla, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Linda demokrasia, uongozi tushiriki, Haki kujielezea, wachotaka na hutaki, Change naweza tetea, demokrasia haki, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili Tena adili usawa, mgao rasilimali, Bajeti inapogawa, isawazishe ratili, Idara zilizoundwa, faidi kila mahali, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Tuwe na uadilifu, twache tamaa ya hongo, Tusiwe na uadilifu, wa kuwa watu waongo, Tukomeshe uhalifu, kisha tuache maringo, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Ubinafsi si adili, ila ni kusaidiya, Ukiwa nayo maali, asiyenacho patiya, Kama mtu mswahili, ubinafsi achiya, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. Na invyoelezea, katiba ni kielezi, Tutii kwa mazoea, hadi kijacho kizazi, Kwa hayo nitawachia, hiyo ya ziada kazi, Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. MASWALI
MAJIBU
SOMA SHAIRI LIFUATALO KISHA UJIBU MASWALI MODEL25122022001
Ulimwengu ulimwengu, ulimwengu naratibu
Yaliyo kichwani mwangu, nataka kuyatubu Wayasome ndu zangu, wa mbali na wa karibu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
Ulimwengu ni kiwanja, cha wenye raha na tabu
Wengine wanajikonja, kwa wengine ni adhabu Kucha na kutwa twahanja, kutafuta matulubu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
Ni uwanja wa balaa, aliniusia babu
Mna mambo yamejaa, ya faraja na kusibu Na machache ya kufaa, ila mengi ya udubu Cha wenye raha na tabu,ulimwengu ni kiwanja.
Ni kiwanja cha Amina,Saidi Ali Rajabu
Wengine kitu hatuna, tunaishia kababu Wale wamejaza sana, wanashindwa kuhesabu Cha wenye raha na tabu, Ulimwengu ni kiwanja.
Ni uwanja wa urongo, na kweli pia ajabu
Kichwa hudanganya shingo, tumbo kiuno chasibu Usitumai ubongo, wa nduguyo na swahibu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
Ni uwanja wa walevi, pombe kwao ni dhahabu
Mara vile mara hivi, wakilewa majudhubu Maneno ya kiujuvi, hujipaka hata shabu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
Ni kiwanja wenye dini, wamtiio wahabu
Mashekhe msikitini, humo humfanya muhibu Mapadiri kanisani, huvihubiri vitabu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
Ni uwanja wa malofa, lofa mtu mwenye tabu
Kusema sana kashifa na moyo kisebusebu Tunakaribia kuja, kwa kushindwa kujimudu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
Ni uwanja wa faraja, alowajali habibu
Na wengine sitotaja, msinambe ninagubu Ni uwanja wa viroja, vigumu kuvikutubu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. maswali(a) Lipe shairi hili anwani ifaayo. (alama 1)
Ulimwengu ni kiwanja
Changamoto ulimwenguni 1 x 1 = alama 1 (b) kwa kutoa mfano, eleza mbinu zozote mbili za lugha zilizotumika katika shairi.(alama 2)
(b) Istiara/ jazanda – ulimwengu ni kiwanja
Msemo – kutwa kuchwa Ukinzani/tanakuzi – wenye raha na tabu Uhuishaji – Kichwa kudanganya shingo (zozote 2x1 = alama 2) (c) Eleza jinsi uhuru wa mshairi ulivyotumika katika shairi. (alama 2)
(c) Inkisari – naratibu – ninaratibu
Ndu zangu – ndugu zangu. Kuboronga lugha – wenye kitu hatuna – wengine hatuna kitu Utohozi – shehe – sheikh Padre – padre (2 x 1 = 2) (d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha tutumbi. (alama 4)
(d) babu alimshauri kuwa ulimwengu ni uwanja wa balaa ulionjaa mambo ya faraja na kusibu. Pia alisema kuwa kuna machache ya kufaidi na mengi ya kuudhi. Kwa hivyo ulimwengu ni kiwanja kwa walio na raha na walio na taabu.
(4x1 = alama 4) (e)Taja na ueleze bahari zozote mbili zilizotumika katika shairi hili.(alama 2)
(e) (i) Tarbia – mishororo minne kwa kila ubeti
(ii) Mathnawi – vipande viwili kwa kila mshororo (iii) Pindu – sehemu ya mwisho kuanzia ubeti unaofuata. (iv) Ukara – vina vya mwisho vinatirirka na vya kati havitiririki. (2x1 = alama 1) (f) Eleza umbo la shairi hili. (alama 4)
(f) (i) Mishororo minne kwa kila ubeti
(ii) Vipande viwili kwa kila mshororo – ukwapi na utao. (iii) Lina beti tisa. (iv) Vina vya mwisho vinatiririka na vya kati vinabadilika (v) Lina kibwagizo – che wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. (vi) mizani ni 8,8 kwa kila mshororo 4x1 = 4 (g) Eleza toni ya shairi hili. (alama 1)
(g) masikitiko (alama 1)
(h) Fafanua dhamira ya mshairi. (alama 2)
(h) Kufahamisha watu hali ilivyo ulimwenguni. Kwamba kuna mazuri na mabaya ili wajihadhari. (1x2= 2)
(i) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi.(alama2)
|
AuthorAtika School Team Archives
January 2023
Categories
All
|